Loading...

Hatima kesi ya kuingiza vifaa vya mawasiliano leo

Loading...
Hatima kesi ya kuingiza vifaa vya mawasiliano leo - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Hatima kesi ya kuingiza vifaa vya mawasiliano leo, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Hatima kesi ya kuingiza vifaa vya mawasiliano leo
link : Hatima kesi ya kuingiza vifaa vya mawasiliano leo

soma pia


Hatima kesi ya kuingiza vifaa vya mawasiliano leo


Grace Gurisha

RAIA wawili wa India wanaotuhumiwa kuingilia mawasiliano ya kimataifa bila kibali cha Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) na kuisababishia Serikali hasara ya Sh bilioni 4.3 wanatarajiwa kupandishwa kizimbani leo kwenye Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Dar es Salaam, kusikiliza hatua ya upelelezi ilipofikia.

Washitakiwa hao ni Kalrav Patel (37) mkazi wa Mazizini, Zanzibar na Kumal Ashar (59) mkazi wa Mkunazini pia Zanzibar.

Kesi hiyo inatarajiwa kutajwa mbele ya Hakimu Mfawidhi, Cyprian Mkeha, ambapo awali upande wa Jamhuri ulidai kuwa upelelezi wa kesi hiyo haujakamilika na kuomba siku nyingine ya kukamilisha upelelezi.

Katika mashitaka ya kwanza, washitakiwa hao wanatuhumiwa kuingiza  nchini vifaa vya mawasiliano bila kibali, katika tarehe zisizofahamika   mwaka juzi wakiwa Zanzibar ambako waliingiza vifaa vya mawasiliano ya sauti katika intaneti (VoIP) yenye namba 0030F1001903 na Cisco Router namba 12F1070C204574 bila kibali cha TCRA.

Ilidaiwa katika mashitaka ya pili kuwa Patel na Ashar katika tarehe zisizofahamika Zanzibar, waliweka au walisimika vifaa hivyo vya mawasiliano bila kibali cha TCRA.

Katika mashitaka ya tatu wanatuhumiwa kutumia vifaa vya mawasiliano ambavyo havijathibitishwa na TCRA, ambapo walitenda kitendo hicho kati ya Februari 25 na Aprili 18 mwaka jana Zanzibar.

Hakimu Mkeha aliwaeleza washitakiwa kuwa Mahakama hiyo haina mamlaka ya kusikiliza kesi hiyo hivyo kutotakiwa kujibu chochote wala kupewa masharti ya dhamana, kwani Mahakama Kuu ndiyo inahusika na dhamana yao. 


Hivyo makala Hatima kesi ya kuingiza vifaa vya mawasiliano leo

yaani makala yote Hatima kesi ya kuingiza vifaa vya mawasiliano leo Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Hatima kesi ya kuingiza vifaa vya mawasiliano leo mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/04/hatima-kesi-ya-kuingiza-vifaa-vya.html

Subscribe to receive free email updates:

0 Response to "Hatima kesi ya kuingiza vifaa vya mawasiliano leo"

Post a Comment

Loading...