Loading...

Kawambwa aomba fedha za hospitali

Loading...
Kawambwa aomba fedha za hospitali - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Kawambwa aomba fedha za hospitali, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Kawambwa aomba fedha za hospitali
link : Kawambwa aomba fedha za hospitali

soma pia


Kawambwa aomba fedha za hospitali


Joyce Kasiki, Dodoma

Shukuru Kawambwa
MBUNGE wa Bagamoyo, Dk Shukuru Kawambwa (CCM), ameiomba Serikali kupeleka fedha kwenye Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo kujenga jingo la kitengo cha wagonjwa wa nje (OPD) la hospitali ya wilaya hiyo.

Mbunge huyo alitoa kauli hiyo jana alipouliza swali la nyongeza bungeni akihoji Serikali kama itakuwa tayari kupeleka fedha kwa ajili hiyo akisema jingo hilo linahitaji kujengwa upya na si kufanyiwa ukarabati.

Awali katika swali la msingi, Dk Kawambwa alitaka kujua mpango wa Serikali kuboresha huduma za afya katika hospitali hiyo kwa kuhakikisha upatikanaji wa miundombinu bora, vitendea kazi na kuiongeza watumishi na dawa za kutosha.

"Kwa muda mrefu sasa huduma za afya katika hopsitali ya wilaya ya Bagamoyo ni dhaifu sana kutoka na upungufu wa miundombinu, vitendea kazi, uhaba wa watumishi na ukosefu wa dawa, Serikali ina mpango gani wa kuboresha huduma za afya katika hospitali hiyo?" Alihoji Dk Kawambwa

Akijibu, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Selemani Jafo alisema katika mwaka wa fedha wa 2017/18, Serikali imetenga Sh 1,465,740,000 za kuboresha huduma za afya katika hospitali hiyo ikiwa ni pamoja na kuboresha miundombinu na upatikanaji dawa na vifaa tiba.

"Vile vile, zimetengwa Sh milioni 185 kwa mwaka wa fedha 2017/18 kutokana na ruzuku ya maendeleo kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya vituo vya kutolea huduma za afya, Sh 59,790,600 kutokana na mapato ya ndani kwa ajili ya upanuzi wa wodi ya wazazi, ukarabati wa OPD, eneo la kuhudumia wagonjwa wa dharura na kumalizia ukarabati wa wodi ya wanaume," alisema Jafo.

Aidha, alisema Serikali imetoa kibali cha kuajiri madaktari na watumishi wengine wa afya huku Halmashauri hiyo pia ikipewa kipaumbele.


Hivyo makala Kawambwa aomba fedha za hospitali

yaani makala yote Kawambwa aomba fedha za hospitali Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Kawambwa aomba fedha za hospitali mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/05/kawambwa-aomba-fedha-za-hospitali.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Kawambwa aomba fedha za hospitali"

Post a Comment

Loading...