Loading...

Serikali Yakusudia Kujenga Magereza Maeneo ya Kilimo

Loading...
Serikali Yakusudia Kujenga Magereza Maeneo ya Kilimo - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Serikali Yakusudia Kujenga Magereza Maeneo ya Kilimo, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Serikali Yakusudia Kujenga Magereza Maeneo ya Kilimo
link : Serikali Yakusudia Kujenga Magereza Maeneo ya Kilimo

soma pia


Serikali Yakusudia Kujenga Magereza Maeneo ya Kilimo

Mwambawahabari
Na Nuru Juma-MAELEZO
Serikali inamkakati wa kuhakikisha inajenga Magereza   katika maeneo yenye uzalishaji mkubwa wa kilimo ambayo pia yana ukubwa wa kutosha ili kazi ya kuwarekebisha wafungwa iwe rahisi kufanyika huku shughuli za uzalishaji zikiwa zinaendelea.
Hayo yamesemwa leo Bungeni Mjini Dodoma na Waziri wa Mambo ya Ndani ya nchi Mhe. Mwigulu Nchemba alipokuwa akijibu swali la Mhe Devotha Minja Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Morogoro.
 “Magereza hayo yatajengwa katika maeneo yenye Kilimo  na yatakuwa  ni kwa ajili ya watu waliokwisha hukumiwa huku yale Magereza ya mijini yawe kwa ajili ya mahabusu tu ili wawe karibu na Mahakama,”alisema Mwigulu.                  
 Aliongeza kuwa mkakati huo wa Serikali ni wa muda mrefu na wanahitaji kufanya hivyo ili kurahisisha shughuli za maendeleo zinazofanywa na wafungwa na pia kupunguza msongamano wa wafungwa katika Magereza.Hili pia linatokana na tamko la Mh.Rais Dkt John Pombe Magufuli alilowahi kulitoa hivi karibuni kuwa wafungwa wako katika kutumikia adhabu hivyo wanatakiwa kufanya kazi hasa za kilimo ili kwanza kujipatia chakula na sio kukaa tu bure na kusubiri kila kitu wafanyiwe na serikali.
Aliongeza kuwa Serikali ina mkakati wa kutumia bajeti inayotengwa na nguvu kazi wanayoipata kutoka kwa wataaalam walionao kwa upande wa askari Magereza na wafungwa ili kukarabati Magereza chakavu na kujenga nyumba za askari.
Aidha alibainisha kuwa suala la kukatwa kwa umeme katika Magereza, nyumba za askari,pamoja na maeneo  na maeneo mengine ya kambi za Jeshi la Polisi na Magereza limeshafanyiwa kazi na serikali kwa kupitia  hazina imekwishatoa fedha kwa ajili ya kutatua tatizo hilo.
Mheshimiwa Waziri aliliambia Bunge kuwa sheria zimeainisha baadhi ya haki za mfungwa zikiwemo huduma za afya kwa wakati,kupewa chakula, uhuru wa kutembelewa na ndugu zake na kupata mawasiliano kwa kusoma magazeti,kusikiliza taarifa za habari na kuandikiwa barua na ndugu zao,haki ya kukata rufaa ikiwa hakuridhika na hukumu yake, malazi safi na yakutosha pamoja na kushiriki michezo mabalimbali.


Hivyo makala Serikali Yakusudia Kujenga Magereza Maeneo ya Kilimo

yaani makala yote Serikali Yakusudia Kujenga Magereza Maeneo ya Kilimo Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Serikali Yakusudia Kujenga Magereza Maeneo ya Kilimo mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/05/serikali-yakusudia-kujenga-magereza.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Serikali Yakusudia Kujenga Magereza Maeneo ya Kilimo"

Post a Comment

Loading...