Loading...

Acacia wakutana na Rais Magufuli Ikulu leo, wakubali kulipa fedha wanazodaiwa

Loading...
Acacia wakutana na Rais Magufuli Ikulu leo, wakubali kulipa fedha wanazodaiwa - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Acacia wakutana na Rais Magufuli Ikulu leo, wakubali kulipa fedha wanazodaiwa, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Acacia wakutana na Rais Magufuli Ikulu leo, wakubali kulipa fedha wanazodaiwa
link : Acacia wakutana na Rais Magufuli Ikulu leo, wakubali kulipa fedha wanazodaiwa

soma pia


Acacia wakutana na Rais Magufuli Ikulu leo, wakubali kulipa fedha wanazodaiwa




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli amekutana na kufanya mazungumzo na Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acacia Mining Limited Prof. John L. Thornton na kukubaliana kuwa kampuni hiyo ipo tayari kufanya mazungumzo na Serikali ya Tanzania ili kulipa fedha ambazo Tanzania imezipoteza kutokana na kampuni hiyo kuendesha shughuli zake hapa nchini.

Prof. John L. Thornton ambaye amesafiri kwa ndege binafsi kutoka nchini Canada hadi Tanzania amekutana na Mhe. Rais Magufuli leo Juni 14, 2017 Ikulu Jijini Dar es Salaam na mazungumzo yao yamehudhuriwa na Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Ian Myles na Waziri wa Sheria na Katiba Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi.

Baada ya Mazungumzo hayo Prof. John L. Thornton amesema kampuni yake ipo tayari kufanya mazungumzo na Tanzania yatakayozingatia maslahi ya pande zote mbili na pia ipo tayari kulipa fedha zote ambazo inapaswa kulipa kwa Tanzania.

Kwa upande wake Mhe. Rais Magufuli amesema Serikali inakaribisha mazungumzo hayo na itaunda jopo la wataalamu watakaofanya majadiliano na kampuni ya Barrick Gold Corporation ili kufikia makubaliano ya kulipwa fedha zinazodaiwa na namna kampuni hiyo itakavyoendesha shughuli zake nchini maslahi ya pande zote mbili.

Mhe. Rais Magufuli amesema pamoja na kukubali kulipa fedha zinazodaiwa Prof. John L. Thornton amekubali kushirikiana na Tanzania kujenga mtambo wa kuchenjulia dhahabu (smelter) hapa nchini.

Wakati huo huo, Mhe. Rais Magufuli amevionya vyombo vya habari vinavyowataja Marais wastaafu Mhe. Benjamin William Mkapa na Mhe. Jakaya Mrisho Kikwete na kuwahusisha na taarifa za kamati mbili za uchunguzi wa madini yaliyo katika makontena yenye mchanga wa madini (Makinikia) ambao ripoti zimekabidhiwa kwake na kamati hizo.

“Nimesoma ripoti zote mbili hakuna mahali ambapo Mzee Mkapa na Mzee Kikwete wametajwa, vyombo vya habari viache kuwachafua hawa wazee, wamefanya kazi kubwa ya kulitumikia Taifa letu, viwaache wapumzike” amesema Mhe. Rais Magufuli.

Gerson Msigwa
Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais, IKULU
Dar es Salaam
14 Juni, 2017


Hivyo makala Acacia wakutana na Rais Magufuli Ikulu leo, wakubali kulipa fedha wanazodaiwa

yaani makala yote Acacia wakutana na Rais Magufuli Ikulu leo, wakubali kulipa fedha wanazodaiwa Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Acacia wakutana na Rais Magufuli Ikulu leo, wakubali kulipa fedha wanazodaiwa mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/06/acacia-wakutana-na-rais-magufuli-ikulu.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Acacia wakutana na Rais Magufuli Ikulu leo, wakubali kulipa fedha wanazodaiwa"

Post a Comment

Loading...