Loading...

Watoto wanakuja kuchukua mkono wa Idd au wametumwa kuomba?

Loading...
Watoto wanakuja kuchukua mkono wa Idd au wametumwa kuomba? - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Watoto wanakuja kuchukua mkono wa Idd au wametumwa kuomba?, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Watoto wanakuja kuchukua mkono wa Idd au wametumwa kuomba?
link : Watoto wanakuja kuchukua mkono wa Idd au wametumwa kuomba?

soma pia


Watoto wanakuja kuchukua mkono wa Idd au wametumwa kuomba?

Na Ummu Anfaal

Mkono wa Eid wapendwa ndugu zangu katika imaan.  

Alhamdulillah Tumshukuru Allah Subhaanahu wata'ala atutakabalie swaumu zetu na tulipoteleza  atughufirie na atujaalie Rehma za Mwezi wa Ramadhan. Na Neema kwenye Eid.   

Awali  maisha ya mwezi mtukufu wa Ramadhaan ni mazuri sana kwa hiyo tusiyawache uwe ndio mfumo wetu.  Maaswi yalozuiliwa ndio tuwe tumeyafukia. Tuishi kama mwezi mtukufu. Na nina iman wengi wetu hatukuwa kwenye israaf kutokana na hali ya maisha.  Kwa hiyo tutaweza kujimudu na mlo mmoja .  Hakuna ulazima wa milo mitatu.  

Inshaa Allah nimependa kuwasilisha hili nililolishuhudia   muda mchache. Nimefikiwa na ugeni wa takriban watoto watano katika vigurupu tofauti.  

Walibisha hodi  na kusema mkono wa eid.  Siwajui na hawanijui, lao ni kuja kuchukua eid. 

Nilipowauliza  wanatokea wapi ? Wamenijibu  Kwa Alamshaa ni kipande na nilipokaa. Hawa watoto hawana kosa . Kosa lipo kwa wazazi.   Sisi tulikulia huko miaka ya nyuma. Na hali ya maisha haikuwa kama sasa.  Kila kitu kilikuwa tunu. Sasa vitu vimejaa kila mahala hakuna jipya. Ni kweli hali za maisha ni ngumu lakini wazazi tunapaswa kuwafundisha watoto wetu maadili mema .

Hii  tabia ya kuranda na kuomba si nzuri.  Eid wanatembeleana ndugu jamaa na marafiki.  Ningependa wahusika hasa viongozi wetu wa dini kungetengwa gawio kwa wasiojiweza kwenda sehemu maalum kula eid na mwenye nacho au anotaka ku tabaruk awasilishe huko. Huu mfumo wa sasa wa kupita kuomba tusiukodolee macho tu  na kunong'ona na kusengenya watoto .upo toka muaka michache ya nyuma lakini kila tukenda mambo yanazidi.  

Namuunga mkono sheikh NYUNDO watoto wanatumwa kwenda KUOMBA.  Haileti taswira nzuri .   Allah atujaalie kheri .  Amiin.                            


Hivyo makala Watoto wanakuja kuchukua mkono wa Idd au wametumwa kuomba?

yaani makala yote Watoto wanakuja kuchukua mkono wa Idd au wametumwa kuomba? Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Watoto wanakuja kuchukua mkono wa Idd au wametumwa kuomba? mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/06/watoto-wanakuja-kuchukua-mkono-wa-idd.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Watoto wanakuja kuchukua mkono wa Idd au wametumwa kuomba?"

Post a Comment

Loading...