Loading...

British Council  yawaalika watanzania wote wanaopenda kujifunza kiingereza

Loading...
British Council  yawaalika watanzania wote wanaopenda kujifunza kiingereza - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa British Council  yawaalika watanzania wote wanaopenda kujifunza kiingereza, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : British Council  yawaalika watanzania wote wanaopenda kujifunza kiingereza
link : British Council  yawaalika watanzania wote wanaopenda kujifunza kiingereza

soma pia


British Council  yawaalika watanzania wote wanaopenda kujifunza kiingereza

Na Karama Kenyunko Globu ya jamii.

TAASISI ya Elimu, British Council  inawaalika watanzania wote wanaopenda kujifunza kiingereza kujitokeza kwa wingi kwenye banda lao la sabasaba kwa ajili ya kufanya mtihani na kupunguza garama.

Taasisi hiyo inatumia maonesho ya 41 ya kimataifa ya Biashara  ya  Dar e Salaam (DITF) kutoa mitihani ya kiwango cha lugha ya Kiingereza bure kwa wananchi  wanaohitaji,lengo likiwa ni kujipima ufahamu wao. Meneja wa Maendeleo na Biashara kutoka British Council, Amata Bosco amesema hayo leo katika maonyesho yanayofanyika katika barabara ya Kilwa.
 Mkurugenz wa British Council Nchini, Angela Hennely akizungumza na waandish was habari katika mkutano huo.

Amesema kwa Tanzania kuna uhitaji  mkubwa wa kukuza lugha ambapo watu wengi wamejitokeza katika banda hilo kwa ajili ya kufanya mitihani hiyo yenye kujipima kiwango chao cha Kingereza. 
Amesema  mtihani wa kiwango unaofanyika katika maonesho hayo ni bure unapunguza garama kubwa wa watu wanaopenda kujifunza kiingereza kwa kuwa ukifanyia mtihani huo shuleni kwao unalazimika kulipia sh.48,000.

"kufanyika kwa mitihani hii ya kiwango katika maonesho kutasaidia watanzania walio wengi kuokoa kiwango cha fedha ambacho hukitumia wakati wa kawaida kwa kwenda kusoma katika taasis hiyo", amesema.
"Lengo kubwa la kufanya mtihani huu bure ni  kuhamasiha watu kujiandikisha kwa wingi katika kozi mbalimbali zitolewazo na taasisi hiyo ili kuboresha lugha ya Kiingereza.  Aidha amesema Taaasisi hiyo inawaunganisha watu na Uingereza katika ubunifu na vitu mbalimbali napia kujifunza masuala mbalimbali kutoka nchi hiyo. 

Amata amewaasa, watanzania  wanaopenda kujifunza ama kufundisha  Kiingereza kujitokeza kwa wingi, kufanya mitihani,  katik taasisi hiyo kwani ni  eneo muhimu la kuanzia na kwamba ndio maana wanatumia maonesho hayo maarufu kama sabasaba kwa ajili kuweza kuwafikia walio wengi Zaidi. 

" Mtihani huu wa kiwango wa  Kiingereza unafanyika kila siku ya maonesho na watu wengi wamekuwa wakifika hapa wakiwepo wenye kiwango cha chini, cha katikati na hata kiwango cha juu lakini pia wapo wasiojiamini katika kuzungumza lugha hiyo ambao na wamekuwa wakifika. 


Hivyo makala British Council  yawaalika watanzania wote wanaopenda kujifunza kiingereza

yaani makala yote British Council  yawaalika watanzania wote wanaopenda kujifunza kiingereza Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala British Council  yawaalika watanzania wote wanaopenda kujifunza kiingereza mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/07/british-council-yawaalika-watanzania.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "British Council  yawaalika watanzania wote wanaopenda kujifunza kiingereza"

Post a Comment

Loading...