Loading...

Mpinga wa Trafiki awa Kamanda wa Mkoa

Loading...
Mpinga wa Trafiki awa Kamanda wa Mkoa - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Mpinga wa Trafiki awa Kamanda wa Mkoa, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Mpinga wa Trafiki awa Kamanda wa Mkoa
link : Mpinga wa Trafiki awa Kamanda wa Mkoa

soma pia


Mpinga wa Trafiki awa Kamanda wa Mkoa


Mwandishi Wetu

Kamanda Mpinga
MAAGIZO ya Rais John Magufuli kwa Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini Simon Sirro yameanza kutekelezwa. Hivyo ndivyo unavyoweza kusema baada ya jana Mkuu huyo wa Polisi kufanya mabadiliko yaliyogusa wadhifa wa kitaifa  kwenye Jeshi hilo.

Katika mabadiliko hayo, IGP Sirro amemng’oa kwenye nafasi yake aliyekuwa Mkuu wa Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohammed Mpinga na kumteua kuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya.

Akizungumza baada ya kumwapisha Sirro hivi karibuni Ikulu, Dar es Salaam, Rais Magufuli alimtaka kusafisha Jeshi hilo lililokumbwa na changamoto za kiutendaji yakiwamo matukio ya ujambazi na mauaji ya askari wake na raia Kibiti, Pwani.

Taarifa ya Jeshi hilo iliyotolewa jana na Msemaji wake, Barnabas Mwakalukwa ilisema Sirro amembadilisha kituo cha kazi na nafasi yake inachukuliwa na Fortunatus Musilimu ambaye alikuwa Mkuu wa Operesheni kwenye kikosi hicho.

Kabla ya uteuzi huo wa jana, Musilimu alikuwa akikaimu nafasi aliyokuwa nayo Mpinga huku ikielezwa kuwa Mkuu huyo wa zamani wa Trafiki alikuwa likizo.

Kwa mujibu wa mabadiliko hayo, aliyekuwa Kamanda wa Polisi wa Mkoa wa Mbeya, Dhahiri Kidavashari, amehamishiwa Makao Makuu ya Upelelezi.

Hata hivyo, Msemaji huyo wa Polisi alisema uhamisho huo ni wa kawaida katika alichoeleza kuwa ni kuboresha utendaji kazi zao kwa mujibu wa kanuni, taratibu na miongozo ya Polisi.

Mpinga alipotafutwa kuzungumzia mabadiliko hayo, simu yake iliita muda mrefu bila majibu.
hicho kwa zaidi ya miaka mitano na nyota yake iling’ara alipokaimu akiwa na aliyekuwa Mkuu wa Kikosi hicho, marehemu James Kombe.

Alipotakiwa kuzungumzia uamuzi wa Sirro kumpandisha cheo aliyekuwa   Musilimu, alisema atazungumza baada ya kukabidhiwa ofisi na kwa sasa aachwe kwanza.

“Ndiyo nimejua leo, jamani niacheni nikabidhiwe ofisi ndipo nitazungumza mikakati yangu. Bado mwenzangu yuko ofisini,” alisema.



Hivyo makala Mpinga wa Trafiki awa Kamanda wa Mkoa

yaani makala yote Mpinga wa Trafiki awa Kamanda wa Mkoa Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Mpinga wa Trafiki awa Kamanda wa Mkoa mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/07/mpinga-wa-trafiki-awa-kamanda-wa-mkoa.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Mpinga wa Trafiki awa Kamanda wa Mkoa"

Post a Comment

Loading...