Loading...
title : MWANJALE NAHODHA MPYA WA SIMBA,MKUDE APIGWA CHINI
link : MWANJALE NAHODHA MPYA WA SIMBA,MKUDE APIGWA CHINI
MWANJALE NAHODHA MPYA WA SIMBA,MKUDE APIGWA CHINI
SIMBA SPORTS CLUB
DAR ES SALAAM
29-7-2017
TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI.
______________
Benchi la ufundi la klabu ya Simba,chini ya kocha wake mkuu Joseph Omog limefanya marekebisho kwenye eneo la unahodha wa timu.
Katika marekebisho hayo yaliyoridhiwa na uongozi wa klabu,beki wa kimataifa Mzimbabwe Method Mwanjale ameteuliwa kuwa nahodha mpya wa timu ya Simba,akichukua nafasi ya Jonas Mkude atakaendelea kuwa mchezaji mwandamizi kwenye kikosi hicho,ambacho kwa sasa kipo nchini Afrika kusini kujiandaa na msimu mpya unaotarajiwa kuanza mwezi ujao.
Kwenye mabadiliko hayo ya kawaida, benchi la ufundi pia limewateua Mchezaji bora wa ligi kuu ya Tanzania na klabu ya Simba kwa msimu huu,Mohammed Hussein(Tshabalala)na John Raphael Boko kuwa manahodha wasaidizi wa timu hiyo.
Klabu inamshukuru sana Nahodha wake kwenye msimu uliopita na mchezaji wake mwandamizi,Jonas Mkude kwa kazi nzuri alioifanya muda wote alipokuwa Nahodha wa Timu.
Kwa sasa kikosi chetu kinaendelea na mazoezi na kila kitu kinakwenda vema huko kambini Eden Vale Johannesburg nchini Afrika kusini.
IMETOLEWA NA..
HAJI S MANARA
MKUU WA HABARI WA SIMBA SC
SIMBA NGUVU MOJA
Hivyo makala MWANJALE NAHODHA MPYA WA SIMBA,MKUDE APIGWA CHINI
yaani makala yote MWANJALE NAHODHA MPYA WA SIMBA,MKUDE APIGWA CHINI Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MWANJALE NAHODHA MPYA WA SIMBA,MKUDE APIGWA CHINI mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/07/mwanjale-nahodha-mpya-wa-simbamkude.html
0 Response to "MWANJALE NAHODHA MPYA WA SIMBA,MKUDE APIGWA CHINI"
Post a Comment