Loading...

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco afanya ziara nchini

Loading...
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco afanya ziara nchini - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco afanya ziara nchini, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco afanya ziara nchini
link : Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco afanya ziara nchini

soma pia


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco afanya ziara nchini


Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kutoka Serikali ya Ufalme wa Morocco Mhe.Mounia Boucetta na ujumbe wake wametembelea Wizara leo tarehe 13 Julai, 2017 na kufanya mazungumzo na mwenyeji wake Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt. Suzan Kolimba katika ukumbi wa Wizara, Dar es Salaam. Mhe. Mounia Boucetta yupo nchini kwa ziara ya kikazi tangu tarehe 12 Julai, 2017.

Lengo la ziara hiyo ni kufuatilia utekelezaji wa Maazimio na makubaliano ya Ushirikiano kati ya taasisi za Tanzania na Morocco katika sekta mbalimbali, yaliyosainiwa wakati wa ziara ya Mfalme Mohammed VI wa Morocco nchini Tanzania tarehe 23 – 25 Octoba, 2016. 

Itakumbukwa katika ziara hii jumla ya mikataba 21 ya Ushirikiano katika maeneo mbalimbali ilisainiwa. Mikataba hiyo ni katika masuala yafuatayo; Masuala ya Usafiri wa Anga, Kilimo na Uvuvi, Nishati, Utalii, Viwanda Usafiri wa Reli, Biashara, Masuala ya Bima, Masuala ya Afya, Masuala ya Gesi, Masuala ya Siasa, Uchumi, Sayansi na Utamaduni. 

Aidha Mheshimiwa Mfalme Mohamed VI aliahidi mambo makuu matatu

· Ujenzi wa msikiti mkubwa wa kisasa jijini Dar es salaam
· Ujenzi wa uwanja wa kisasa wa mpira mjini Dodoma
· Kuanzisha programu ya mafunzo kwa maafisa wa majeshi yetu ya ulinzi na usalama

Tangu ziara hiyo ifanyike Serikali ya Ufalme wa Morocco, katika kuimarisha urafiki na ushirikiano ilifungua Ubalozi wake jijini Dar es salaam, na Mwezi Februari, 2017 Mheshimiwa Balozi Abdelillah Benryane aliwasilisha hati zake za utambulisho Nchini.

Mhe. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt.Suzan Kolimba (kulia) akiwa katika mazungumzo na Mhe. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa kutoka Ufalme wa Morocco Mhe.Mounia Boucetta katika ukumbi wa Wizara- Dar es Salaam, tarehe 13 Julai,2017. 
Mhe. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Dkt.Suzan Kolimba akipokea zawadi kutoka kwa, Mhe. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Ufalme wa Morocco baada ya mazungumzo. 
Mhe. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt.Suzan Kolimba, Mhe. Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa wa Ufalme wa Morocco na ujumbe wake, wengine ni wataalam kutoka Wizarani wakiwa katika picha ya pamoja baada ya mazungumzo .



Hivyo makala Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco afanya ziara nchini

yaani makala yote Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco afanya ziara nchini Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco afanya ziara nchini mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/07/naibu-waziri-wa-mambo-ya-nje-wa-morocco.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Morocco afanya ziara nchini"

Post a Comment

Loading...