Loading...

Wakili: Sethi kupoteza maisha asipotibiwa haraka

Loading...
Wakili: Sethi kupoteza maisha asipotibiwa haraka - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Wakili: Sethi kupoteza maisha asipotibiwa haraka, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Wakili: Sethi kupoteza maisha asipotibiwa haraka
link : Wakili: Sethi kupoteza maisha asipotibiwa haraka

soma pia


Wakili: Sethi kupoteza maisha asipotibiwa haraka

WAKILI wa Utetezi, Joseph Makandege ameieleza Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu kuwa mshitakiwa wa kwanza katika kesi ya uhujumu uchumi na utakatishaji fedha inayomkabili Herbinder Seth kuwa asipotibiwa ipasavyo, puto lililowekwa kwenye tumbo lake linaweza kupasuka na kusababisha kifo.

Makandege alidai hayo jana mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Huruma Shaidi na kueleza mahakama kuwa mshitakiwa huyo alifanyiwa upasuaji na kuwekwa puto tumboni.

Alidai kuwa  katika mashauri yaliyopita, mahakama ilitoa amri mara mbili, zote zikielekeza mshitakiwa huyo apelekwe Hospitali ya Muhimbili lakini haijatekelezwa.

Aliomba mahakama izingatie ugonjwa wa mshitakiwa na iamuru apelekwe moja kwa moja Muhimbili kwani  ndio hospitali ya juu  ya serikali nchini ambayo inategemea kuwa na wataalamu na vifaa stahiki vya ugonjwa unaomkabili.

"Upande wa jamhuri unatambua haya lakini kwa ridhaa yao wao wamempeleka mshitakiwa Amana hospitali. Swali ambalo mahakama isaidie kujibu pamoja na jamhuri, ni  je, kumpeleka mshitakiwa wa kwanza hospitali ya Amana,  magereza na jamhuri wameshindwa kutii amri ya mahakama?," alihoji Makandege.

“Mahakama haikumungunya maneno katika kutoa amri yake, ambapo ilitamka kwenye amri hiyo kwamba mshitakiwa huyo  apelekwe katika hosipitali ya taifa ya Muhimbili, wao kumpeleka Amana wametekeleza amri gani?” Makandege aliendelea kueleza.

Alidai  amri ya mahakama  haijatekelezwa hivyo upande wa mashitaka umekaidi amri hiyo."Mahakama ndio mahala amri zote zitaheshimiwa kwa pande zote mbili kwa kuwa nchi inafuata demokrasia na utawala wa sheria," alidai Makandege.

Makandege alidai kuwa kilichofanyika ni kinyume na amri ya mahakama na kinyume na sheria za magereza kifungu cha 53 (1) ambacho kinatoa fursa kwa mtu yoyote aliyeko gerezani kama anaumwa kufikishwa hospital ili apate matibabu.



Hivyo makala Wakili: Sethi kupoteza maisha asipotibiwa haraka

yaani makala yote Wakili: Sethi kupoteza maisha asipotibiwa haraka Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Wakili: Sethi kupoteza maisha asipotibiwa haraka mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/08/wakili-sethi-kupoteza-maisha.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Wakili: Sethi kupoteza maisha asipotibiwa haraka"

Post a Comment

Loading...