Loading...
title : MUHIMBILI YAPOKEA WATAALAMU 16 KUTOKA CUBA.
link : MUHIMBILI YAPOKEA WATAALAMU 16 KUTOKA CUBA.
MUHIMBILI YAPOKEA WATAALAMU 16 KUTOKA CUBA.
Na; Agness Moshi na Pascal Dotto-MAELEZO.
Hospitali ya Taifa ya Muhimbili (MNH) imepokea wataalamu 16 kutoka nchini Cuba kama moja ya mikakati yake ya kuboresha utoaji huduma za Afya ikiwemo kutoa huduma za kibingwa hapa nchini.
Akiongea na Waandishi wa Habari Jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya,Maendeleo ya jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Dk.Mpoki Ulisubisya alisema kuwa Serikali imepokea madaktari bingwa 6, madaktari bingwa wa usingizi 2, madaktari wa wodi za wagonjwa mahututi 2, Daktari bingwa wa upasuaji wa macho 1, mtaalamu mmoja wa radiolojia pamoja na wauguzi 10 wa vyumba vya wagonjwa mahututi.
“Wataalam hawa mamekuja wakati muafaka, kwasababu kwa kipindi hiki hospitali ya Muhimbili inafanya maboresho ya utoaji huduma , hivyo nina amini uwepo wao hapa kwa miaka miwili, hautakuwa kwa ajili ya kuboresha huduma au kusaidia wagonjwa tu , bali ni nafasi nzuri ya kuwapa ujuzi na mafunzo wataalamu wetu “,alisema Dk.Ulisubisya.
Dk. Ulisubisya amesema kuwa uwepo wa wataalamu hao utaongeza nguvu kazi hususani kwenye utoaji huduma kwa wagonjwa mahututi kwani hospitali hiyo imeongeza vitanda vya wagonjwa mahututi kutoka vitanda 21 hadi 88.
Katibu mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya(katikati) akieleza jambo wakati wa kuwakaribisha wataalamu 16 kutoka nchni Cuba wakiwemo Madaktari Bingwa 6 pamoja na Wauguzi wa Chumba cha uangalizi maalumu kwa wagonjwa mahutiti mapema leo Hospitali ya Taifa Muhimbili Jijini Dar es Salaam kushoto ni kiongizi mkuu wa matibabu nchini Tanzania Dkt. Maylen Lopezi na kulia ni Mkurugenzi mtendaji wa Hospitali ya taifa Muhimbili Profesa Lawrence Museru.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Dkt. Mpoki Ulisubisya akiwa katika picha ya pamoja na wataalamu kutoka Cuba katika hafla ya kuwakaribisha katika Hospitali ya Taifa Muhimbili leo Jijini Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Hivyo makala MUHIMBILI YAPOKEA WATAALAMU 16 KUTOKA CUBA.
yaani makala yote MUHIMBILI YAPOKEA WATAALAMU 16 KUTOKA CUBA. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MUHIMBILI YAPOKEA WATAALAMU 16 KUTOKA CUBA. mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/10/muhimbili-yapokea-wataalamu-16-kutoka.html
0 Response to "MUHIMBILI YAPOKEA WATAALAMU 16 KUTOKA CUBA."
Post a Comment