Loading...

BENKI YA CRDB YAWAPA AHUENI WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

Loading...
BENKI YA CRDB YAWAPA AHUENI WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa BENKI YA CRDB YAWAPA AHUENI WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : BENKI YA CRDB YAWAPA AHUENI WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU
link : BENKI YA CRDB YAWAPA AHUENI WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

soma pia


BENKI YA CRDB YAWAPA AHUENI WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

Ikiwa ni msimu mpya wa ufunguzi wa vyuo mbalimbali nchini, Benki ya CRDB imewapa ahueni kubwa wanafunzi wa elimu ya juu katika vyuo mbalimbali nchini kwa kusogeza huduma za kibenki katika maeneo yanayotumika kufanya usajili wa wanafunzi. Kupitia matawi yake yanayotembea na wakala wa benki (FahariHuduma), Benki ya CRDB imeweza kupeleka huduma za kuweka na kutoa fedha ili kurahisisha malipo mbalimbali yanayofanywa na wanafunzi wakati wanajisajili chuoni ikiwemo kulipia ada na gharama nyingine za chuo.

Ukiondoa huduma za kuweka na kutoa fedha, zoezi la ufunguzi wa akaunti maalum ya wanafunzi ya Scholar limekua likifanyika ili kuwawezesha wanafunzi hususani wale wanaopokea mikopo ya elimu ya juu kuweza kutunza fedha zao kwa usalama. Katika Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM) ambacho kina jumla ya vitivo saba ndani yake, Benki ya CRDB imeweza kusogeza huduma za kifedha katika vitivo vyote saba pamoja na kuwa na tawi na mashine za kutolea fedha katika vitivo vyote.

Akizungumza na mwandishi wetu mmoja wa wanafunzi wa mwaka wa kwanza katika Chuo cha Dodoma Ikupa Mwambene amesema, “tunaishukuru sana Benki ya CRDB kwa kuweza kutusogezea huduma hadi katika vitivo vyetu kwani imeweza kuturahisishia zoezi kufanya usajili na kuokoa muda mwingi”. Nae Afisa Uhusiano wa chuo hiko Bi. Beatrice Baltazar amesema kuwa uwepo wa huduma za benki zinatozolewa na Benki ya CRDB umeweza kuwapa unafuu mkubwa wanafunzi kwa kuwa ilikua ikiwalazimu kwenda nje ya chuo kufata huduma za kibenki kasha kurudi chuoni ili kufanya usajili jambo lililokua linachukua muda mwingi sana.
 Baadhi ya wanafunzi wapya wa Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) wakipatiwa huduma za kuweka na kutoa fedha kutoka Benki ya CRDB kupitia matawi yake yanayotembea na wakala wa benki (FahariHuduma), ili kurahisisha malipo mbalimbali yanayofanywa na wanafunzi wakati wanajisajili chuoni ikiwemo kulipia ada na gharama nyingine za chuo.
 Wakala wa FahariHuduma wa Benki ya CRDB akichukua taarifa kutoka kwa mmoja wa wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dodoma (UDOM) leo wakatika walipowasogezea huduma za kuweka na kutoa fedha ili kurahisisha malipo mbalimbali yanayofanywa na wanafunzi wakati wanajisajili chuoni ikiwemo kulipia ada na gharama nyingine za chuo.
 Baadhi ya wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dodoma wakiendelea kupatiwa huduma kutoka kwa Maafisa wa Benki ya CRDB wa tawi lake linalotembea na wakala wa benki (FahariHuduma),



Hivyo makala BENKI YA CRDB YAWAPA AHUENI WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU

yaani makala yote BENKI YA CRDB YAWAPA AHUENI WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala BENKI YA CRDB YAWAPA AHUENI WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/11/benki-ya-crdb-yawapa-ahueni-wanafunzi.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "BENKI YA CRDB YAWAPA AHUENI WANAFUNZI WA ELIMU YA JUU"

Post a Comment

Loading...