Loading...

KILIMANJARO STARS YAONGEZA WATATU, KULIFUATA KOMBE LA CHALENJI KESHO

Loading...
KILIMANJARO STARS YAONGEZA WATATU, KULIFUATA KOMBE LA CHALENJI KESHO - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa KILIMANJARO STARS YAONGEZA WATATU, KULIFUATA KOMBE LA CHALENJI KESHO, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : KILIMANJARO STARS YAONGEZA WATATU, KULIFUATA KOMBE LA CHALENJI KESHO
link : KILIMANJARO STARS YAONGEZA WATATU, KULIFUATA KOMBE LA CHALENJI KESHO

soma pia


KILIMANJARO STARS YAONGEZA WATATU, KULIFUATA KOMBE LA CHALENJI KESHO

LIFUATA KOMBE LA CHALENJI KESHO

Kocha Mkuu wa timu ya mpira wa miguu ya Tanzania Bara, ‘Kilimanjaro Stars’, Ammy Conrad Ninje, ameongeza nyota watatu katika kikosi chake mara baada ya Baraza la Soka la Afrika Mashariki (CECAFA), kuridhia kuongezwa wachezaji watatu kwa kila timu.
Awali, CECAFA ilihitaji wachezaji 20 tu, lakini sasa wameongeza watatu na kufanya idadi mpya ya wachezaji watakaoshiriki michuano hiyo ya Chalenji kwa mwaka huu kuwa 23.
Wachezaji walioongezwa na Kipa Ramadhani Kabwili kutoka Young Africans ya Dar es Salaam, Amani Kiata  wa Nakuru All Stars ya Kenya na Yahya Zayd kutoka Azam FC ya Dar es Salaam.
Kikosi cha wachezaji 20 wa awali wa Ninje - Kocha wa Daraja ‘A’ la Shirikisho la Mpira wa Miguu Ulaya (UEFA), ni makipa Aishi Manula (Simba SC) na Peter Manyika (Singida United).
Walinzi ni Gadiel Michael (Young Africans), Boniphace Maganga (Mbao FC), Kelvin Yondani (Young Africans), Kennedy Juma (Singida United), Erasto Nyoni (Simba SC) na Mohammed Hussein (Simba SC).
Viungo wa kati ni Himid Mao ambaye ni Nahodha (Azam FC), Jonas Mkude (Simba SC), Hamis Abdallah (Sony Sugar/Kenya), Mzamiru Yassin (Simba SC), Raphael Daud (Young Africans), Shizza Kichuya (Simba SC), Abdul Hilal (Tusker/Kenya) na Ibrahim Ajib (Young Africans).
Washambuliaji ni Mbaraka Yussuph (Azam FC), Elias Maguri (Dhofar/Mascat, Oman), Daniel Lyanga (Fanja FC/Mascat) na Yohana Mkomola (Ngorongoro Heroes). 
Benchi la Ufundi linaundwa na yeye Ninje ambaye ni Kocha Mkuu, Fulgence Novatus (Kocha Msaidizi), Patrick Mwangata (Kocha wa Makipa), Danny Msangi (Meneja), Dkt. Richard Yomba (Daktari wa timu), Dkt. Gilbert Kigadye (Daktari wa Viungo) na Ally Ruvu (Mtunza Vifaa). 
Katika michuano hiyo inayotarajiwa kuanza Desemba 3, mwaka huu, Kilimanjaro Stars imepangwa Kundi ‘A’ pamoja wenyeji Kenya, Rwanda na Libya ambayo ni timu mwalikwa kutoka Kaskazini mwa Afrika.
Kilimanjaro Stars ambayo imewahi kutwaa mara tatu taji hilo la Chalenji tangu kuanzishwa kwake, itaaza kampeni za kurudisha heshima yake dhidi ya Libya katika kundi hilo la A utaofanyika Desemba 3, mwaka huu. 


Hivyo makala KILIMANJARO STARS YAONGEZA WATATU, KULIFUATA KOMBE LA CHALENJI KESHO

yaani makala yote KILIMANJARO STARS YAONGEZA WATATU, KULIFUATA KOMBE LA CHALENJI KESHO Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala KILIMANJARO STARS YAONGEZA WATATU, KULIFUATA KOMBE LA CHALENJI KESHO mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/11/kilimanjaro-stars-yaongeza-watatu.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "KILIMANJARO STARS YAONGEZA WATATU, KULIFUATA KOMBE LA CHALENJI KESHO"

Post a Comment

Loading...