Loading...

WAKULIMA WA KANDA YA ZIWA KUFIKIWA KUPITIA KONGANE

Loading...
WAKULIMA WA KANDA YA ZIWA KUFIKIWA KUPITIA KONGANE - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa WAKULIMA WA KANDA YA ZIWA KUFIKIWA KUPITIA KONGANE, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : WAKULIMA WA KANDA YA ZIWA KUFIKIWA KUPITIA KONGANE
link : WAKULIMA WA KANDA YA ZIWA KUFIKIWA KUPITIA KONGANE

soma pia


WAKULIMA WA KANDA YA ZIWA KUFIKIWA KUPITIA KONGANE

Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imedhamiria na kujizatiti kuhakikisha inachangia kwa kiasi kikubwa katika  kuleta Mapinduzi yenye tija katika Sekta ya Kilimo kwa wakulima wa kanda ya ziwa na Tanzania kwa ujumla ili kusaidia upatikanaji wa fedha na sera nzuri zitakazosaidia maendeleo ya kilimo nchini.

Dhamira hiyo imewekwa wazi na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila wakati akitembelea miradi mbalimbali ya kilimo mkoani Mwanza hivi karibuni.

Bibi Kurwijila alisema kuwa katika kutekeleza mkakati wa kuwafikia wakulima wengi zaidi nchini Benki ya Maendeleo ya Kilimo Tanzania (TADB) imejipanga kutoa huduma kupitia kongane mpya nane (8) ili kuongeza tija kwa wakulima nchini.

“Kongane ni njia ya kimkakati ya kijiografia yenye kujikita katika shughuli za kilimo zinazohusiana, wasambazaji, na taasisi zinazohusishwa katika kujenga usawa wa moja kwa moja miongoni mwa wadau, hivyo ili kukidhi mahitaji ya wakulima nchini, benki ya kilimo itawafikia kupitia njia hii,” alisema.

Aliongeza kuwa kongane ya Kanda ya Ziwa ambayo inajumuisha mikoa ya Mwanza, Kagera, Mara, Shinyanga, Geita na Simiyu itatoa fursa ya ushindani kwa njia endelevu ili kuchagiza uhusiano na ushirikiano katika uongezaji wa thamani hasa katika makundi mbalimbali ya minyororo ya thamani, pamoja na taasisi na mamlaka za udhibiti zinazosaidia sekta ya kilimo nchini.
 Meneja Uendeshaji wa Kiwanda cha Chobo, Bw. Charles Hotar (kulia) akitoa maelezo juu ya uchakataji wa nyama kwenye Kiwanda hicho kwa ugeni kutoka Benki ya Kilimo. Ugeni huo uliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila (wapili kulia).
 Ugeni huo uliongozwa na Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila (wapili kushoto) wakiangalia namna ng’ombe anavyoandaliwa mara baada ya kuchinjwa.
 Meneja Uendeshaji wa Kiwanda cha Chobo, Bw. Charles Hotar (wapili kushoto) akionesha soseji zilizokuwa katika hatua za ufungaji. Wanaomuangalia ni wageni kutoka Benki ya Kilimo.
 Wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi ya TADB wakiangalia bidhaa mbalimbali zinazosindikwa na Kiwanda cha Chobo. Kutoka kushoto ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Benki hiyo, Bibi Rosebud Kurwijila na wajumbe wa Bodi ya Wakurugenzi Bw. Joseph Mutashubilwa (wapili kulia) na Bw. Dome Malosha (kulia).

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA


Hivyo makala WAKULIMA WA KANDA YA ZIWA KUFIKIWA KUPITIA KONGANE

yaani makala yote WAKULIMA WA KANDA YA ZIWA KUFIKIWA KUPITIA KONGANE Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala WAKULIMA WA KANDA YA ZIWA KUFIKIWA KUPITIA KONGANE mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/11/wakulima-wa-kanda-ya-ziwa-kufikiwa.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "WAKULIMA WA KANDA YA ZIWA KUFIKIWA KUPITIA KONGANE"

Post a Comment

Loading...