Loading...
title : HALMASHAURI 174 ZAPATA DAWA ZA KUANGAMIZA MBU WAENEZAO MALARIA
link : HALMASHAURI 174 ZAPATA DAWA ZA KUANGAMIZA MBU WAENEZAO MALARIA
HALMASHAURI 174 ZAPATA DAWA ZA KUANGAMIZA MBU WAENEZAO MALARIA
Kaimu Meneja Mkuu wa Kiwanda cha Kuzalisha Dawa ya Viuadudu vya Mbu waenezao Malaria Tanzania (TBPL), Mhandisi Aggrey Ndunguru (katikati) akitoa taarifa ya utekelezaji mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu baadhi ya Halmashauri zilizopatiwa dawa ya viuadudu vya mbu waenezao malaria, Wilayani Kibaha Mkoani Pwani 17 Desemba, 2017.
Mkuu wa Kitengo cha Mauzo na Masoko wa Kiwanda cha Kuzalisha Dawa ya Viuadudu vya Mbu waenezao Malaria Tanzania (TBPL), Bi. Upendo Ndunguru (kushoto) akifafanua masuala mbalimbali mbele ya Waandishi wa habari (hawapo pichani) kuhusu mikakati wa kiwanda hicho katika kutafuta masoko ndani na nje ya nchi, Wilayani Kibaha Mkoani Pwani, 17 Desemba, 2017.(PICHA ZOTE NA MAELEZO)
Na Mwandishi Wetu, Kibaha-Pwani.
Kiwanda cha kuzalisha Dawa ya Viuadudu vya Mbu waenezao Malari Tanzania (TBPL) kimefanikiwa kusambaza dawa katika Halmashauri zaidi ya 174 nchini zenye viwango vikubwa vya malaria ikiwa ni sehemu ya mpango wa Serikali katika kupambana na ugonjwa wa malaria.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa leo Wilayani Kibaha Mkoani Pwani na Kaimu Meneja Mkuu wa kiwanda hicho, Mhandisi Aggrey Ndunguru, usambazaji wa dawa hizo umefuatia maagizo ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli wakati alipotembelea kiwanda hicho Juni 22 mwaka huu.
Akifafanua kuhusu agizo la Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli, Mhandisi Ndunguru alisema kwamba, Rais alizitaka halmashauri zote nchini kununua dawa hizo kupitia Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI), kwasababu kiwanda hicho kimejengwa na Serikali kwa lengo la kupambana na ugonjwa wa malaria.
“Moja ya mambo ambayo Mhe. Rais alituagiza ni kuhakikisha kwamba kiwanda hiki kinatumika kutengeneza dawa za kuua mbu waenezao malaria na pia alituagiza kwamba halmashauri zote nchini zihakikishe zinanunua dawa hizi, na kwamba Serikali ilitenga shilingi bilioni 250 kwa ajili ya kununulia madawa mbalimbali nchini kwa mwaka huu wa fedha”, alisema Ndunguru.
Hivyo makala HALMASHAURI 174 ZAPATA DAWA ZA KUANGAMIZA MBU WAENEZAO MALARIA
yaani makala yote HALMASHAURI 174 ZAPATA DAWA ZA KUANGAMIZA MBU WAENEZAO MALARIA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala HALMASHAURI 174 ZAPATA DAWA ZA KUANGAMIZA MBU WAENEZAO MALARIA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/12/halmashauri-174-zapata-dawa-za.html
0 Response to "HALMASHAURI 174 ZAPATA DAWA ZA KUANGAMIZA MBU WAENEZAO MALARIA"
Post a Comment