Loading...

OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI

Loading...
OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI
link : OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI

soma pia


OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI

Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Mhe. George Masaju amesema,  kutokana na mchango mkubwa wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu katika maendeleo ya  kiuchumi, usalama, utawala wa sheria na utawala bora, Kuna   umuhimu wa Serikali kuendelea kuiimarisha Ofisi  hiyo.

Ameyasema hayo  wakati akimkaribisha Waziri wa Katiba na Sheria, Mhe Profesa Palamagamba Kabudi kuzindua Baraza la  Wafanyakazi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Uzinduzi wa  baraza hilo  umefanyika siku ya jumatatu katika ukumbi wa mikutano wa Jengo la LAPF  Mkoani Dodoma.

Uzinduzi wa Baraza hilo,  ulitanguliwa  na  uchaguzi wa Katibu na Katibu Msaidizi.  Zoezi la uchaguzi lilisimamiwa na  Katibu Mkuu wa TUGHE Mkoa wa Dodoma Bw. John Mchenya,  Naibu Katibu Mkuu TUGHE Taifa Bi. Jane Mbura na  Afisa Kazi Bi. Razina Tuusa.  Waliochaguliwa kwa kura  za  Siri ni  Wakili wa Serikali Mkuu Monica Mbono ambaye anakuwa  Katibu na  Bw. Michael Masanja anakuwa  Katibu msaidizi.

Mhe. Masaju  akiwa ni  Mwenyekiti wa Baraza la wafanyakazi, ameyataja maeneo ambayo  Serikali  inatakiwa kuendelea kuyaimarisha katika Ofisi ya Mwanasheria Mkuu ni pamoja na,  Raslimali fedha, mafunzo, makazi salama kwaajli ya  mawakili wa serikali na  miundombinu ya ofisi.

“Mhe. Waziri, yapo masuala ya kisera ambayo tunaomba  Serikali  inayashughulikie  ipasavyo ili kuiwezesha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuendelea kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi. Maeneo hayo ni  kuajiri Mawakili wa Serikali na Watumishi wa Kada zingine, kujenga majengo ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu  katika Ofisi  za Wilaya na Mikoa ili  kuokoa fedha inayotumika kulipia pango”. Ameleza Mwanasheria Mkuu.

Kwa upande wa mafunzo,  Mwanasheria Mkuu, ameishauri Serikali  katika  kuwajengea uwezo wa kitaalam Mawakili wa Serikali na  watumishi wenzao katika maeneo ya kipaumbele na kuimarisha maslahi ya mawakili wa serikali na watumishi wote katika Ofisi ya  Mwanasheria  Mkuu wa Serikali.
 
  Mwanasheria Mkuu wa Serikali  Mhe. George Masaju  na  Mwenyekiti wa Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya  Mwanasheria Mkuu akimkaribisha Mhe Waziri wa Katiba na Sheria  kuzindua Baraza  la Wafanyakazi na katika salamu zake alisema ni muhumu kwa Serikali  kuendelea kuiimarisha Ofisi ya Mwanasheria Mkuu kutokana na   umuhimu wake  katika maendeleo ya nchi, kiuchumi, kiusalama, katika utawala wa sheria na katiba
 Waziri wa Katiba na Sheria Mhe. Profesa Paramagamba Kabudi akitabasamu mara baada ya kufungua Baraza la Wafanyakazi wa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali  siku ya jumatatu. Baraza hilo linakutana kwa siku mbili katika ukumbi wa LAPF mkoani Dodoma.
 Wajumbe wa Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Ofisi ya  Mwanasheria Mkuu wa Serikali wakiimba wimbo wa mshikamano wakati wa ufunguzi wa Baraza hilo, wajumbe wa   Baraza ni pamoja na  Mawakili  Wafawidhi wa Serikali, Wakuu wa Divisheni na Vitengo, Wajumbe wa TUGHE na mada mbalimbali zilitolewa wakati wa uzinduzi hao.

HABARI ZAIDI BOFYA HAPA



Hivyo makala OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI

yaani makala yote OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/12/ofisi-ya-mwanasheria-mkuu-wa-serikali.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI YAZINDUA BARAZA LA WAFANYAKAZI"

Post a Comment

Loading...