Loading...
title : Benki ya CRDB yaboresha maslahi ya wafanyakazi wake
link : Benki ya CRDB yaboresha maslahi ya wafanyakazi wake
Benki ya CRDB yaboresha maslahi ya wafanyakazi wake
Benki ya CRDB yasaini mkataba wa hali bora kwa wafanyakazi wake na Chama cha Wafanyakazi wa Taasisi za Fedha, Biashara, Huduma na Ushauri (TUICO), katika hafla iliyofanyika katika hoteli ya Ramada Encore iliyopo katikati ya Jiji la Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Menejimenti ya Benki ya CRDB na Viongozi wa TUICO.
Akizungumza na Waandishi wa habari Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB Dkt. Charles Kimei alisema mbali na kusaidia kuongeza morali na motisha ya utendaji kazi kwa wafanyakazi, mkataba huo wa hali bora utakwenda kusaidia kuongeza ustawi kwa wafanyakazi na familia zao na hivyo kuboresha maisha yao kwa ujumla.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei (katikati) pamoja na Mkuu wa Sekta ya Fedha -TUICO Tanzania, Willy Kibona (kushoto) wakisaini Mkataba wa Makubaliano wa hali bora za Wafanyakazi kati ya Benki ya CRDB na Taasisi ya Fedha, Viwanda, Biashara, Huduma na Ushauri (TUICO) katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es salaam leo Februari 15, 2018. Kulia ni Mkurugenzi wa Rasilimali Watu wa Benki ya CRDB, Dorah Ngaliga.
"Ustawi wa wafanyakazi ni muhimu sana kwetu na tunajitahidi kuhakikisha tunatoa kipaumbele katika hili. Mkataba huu utakuwa ni wa kipindi cha miaka mitatu tangu tarehe ya utiaji saini ambapo kuna mambo 19 ambayo kwa pamoja tumeyaridhia na kuyapitisha”, alisema Dkt. Kimei.
Dkt. Kimei alisema katika mkataba huo wa hali bora kwa wafanyakazi, Benki ya CRDB imetoa kipaumbele katika kuboresha afya za wafanyakazi wake. “Benki ya CRDB imekuwa ikichangia asilimia 100 katika huduma za matibabu kwa wafanyakazi wake, tunajivunia sana kwa hilo. Kutokana na mafanikio na umaarufu wa mpango huu tunaoutumia, tumeamua kuboresha zaidi ahadi yetu kwa wafanyakazi wetu mara nyingine tena, "alisema Dkt. Kimei.
Dkt. Kimei alisema kwa upande wa huduma za afya, wafanyakazi wa Benki ya CRDB sasa wameongezewa huduma nyingine ikiwamo huduma za macho na miwani pamoja na huduma ya matibabu kwa wastaafu na wategemezi wao kupitia Shirika la Bima ya Afya ya Taifa (NHIF). Hii inamaanisha kuwa wafanyakazi wa Benki ya CRDB wataendelea kutibiwa kama bado wapo kazini pindi wakistaafu.
Baadhi ya mambo mengine ambayo yaliridhiwa katika mkataba huo wa hali bora kwa wafanyakazi wa Benki ya CRDB ni pamoja na utaratibu mpya wa uthibitishwaji wa wafanyakazi kazini, utaratibu ulioboreshwa wa kushughulikia migogoro ya kikazi, utaratibu wa likizo ya ugonjwa, utaratibu wa likizo ya uzazi, utaratibu wa mazishi ambapo sasa Benki hiyo itagharamia mazishi ya wazazi wa mfanyakazi, mtoto wa kuzaliwa wa mfanyakazi, au aliyeasiliwa pamoja utaratibu wa utoaji tuzo kwa wafanyakazi wa Benki hiyo.
Akimalizia hotuba yake Dkt. Kimei alisema Benki CRDB pia imeanzisha Kamati za Ustawi wa Wafanyakazi katika matawi yake yote kwa ajili ya kubuni na kuratibu programu na shughuli mbalimbali zinazolenga kukuza ustawi wa wafanyakazi na familia zao.
Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Dkt. Charles Kimei akibadilishana Mkataba wa makubaliano na Mkuu wa Sekta ya Fedha -TUICO Tanzania, Willy Kibona (wa pili kushoto) hali bora za Wafanyakazi kati ya Benki ya CRDB na Taasisi ya Fedha, Viwanda, Biashara, Huduma na Ushauri (TUICO) katika hafla fupi iliyofanyika kwenye Ukumbi wa Hoteli ya Ramada, jijini Dar es salaam leo Februari 15, 2018.
Mkurugenzi wa Masoko, Utafiti na Huduma kwa Wateja wa Benki ya CRDB, Tully Mwambapa akizungumza jambo katika hafla fupi iliyofanyika jijini Dar es salaam leo Februari 15, 2018.
Baadhi washiriki
Hivyo makala Benki ya CRDB yaboresha maslahi ya wafanyakazi wake
yaani makala yote Benki ya CRDB yaboresha maslahi ya wafanyakazi wake Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Benki ya CRDB yaboresha maslahi ya wafanyakazi wake mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/02/benki-ya-crdb-yaboresha-maslahi-ya.html
0 Response to "Benki ya CRDB yaboresha maslahi ya wafanyakazi wake"
Post a Comment