Loading...
title : Dulla Mbambe Mwamaso kupima uzito kesho
link : Dulla Mbambe Mwamaso kupima uzito kesho
Dulla Mbambe Mwamaso kupima uzito kesho
NA CHRISTOPHER LISSA
MABONDIA Dulla Mbambe na Felix Mwamaso kutoka nchini Malawi, kesho watapima uzito tayari kwa kupanda uringoni Februali 14 mwaka.
Mahasimu hao watapima uzito katika Hoteli ya National, Keko, jijini Dar es Salaam.
Mpambano huo unaosubiriwa kwa hamu na wanazi wa masumbwi nchini utapigwa katika Uwanja wa Ndani wa Taifa, jijini Dar e am
Akizungumza, jijini Dar es Salaam, jana, Mwenyekiti wa Chama cha Ngumi za Kulipwa Tanzania (TPBO), Yassin Abdalah ‘Ustadhi’ alisema maandalizi yote yamekamilika ambapo bondia Mwamaso ameingia nchini usiku wa kuamkia leo.
“Kesho watapima uzito katika hoteli ya National, Keko na Siku ya wapendanao ndiyo siku ya siku pale taifa,”alisema Yassin.
Aliongeza; “Huu mpambano ni mkubwa kwani watakuwa wanawania ubingwa wa Afrika Mashariki katika uzito wa kilo 76 na utakuwa ni wa round 10,”
Alisema, mbali na Dulla Mbambe na Mwamaso kupima uzito pia mabondia Mada Maugo na Jackob Mganga pamoja na mabondia wengine wa mapambano ya utangulizi watapima uzito.
Mkurugenzi wa Kampuni ya Respect Entertainment, waandaaji wa mpambano huo, Chief Kiumbe , alisema utakuwa ni mpambano wa kihistoria.
“Onyesho litaanza saa 12:00 jioni na litakuwa ni la kisasi, kutokana na mabondia hao kuwa na historia ya kipekee,”alisema Kiumbe.
Hivyo makala Dulla Mbambe Mwamaso kupima uzito kesho
yaani makala yote Dulla Mbambe Mwamaso kupima uzito kesho Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Dulla Mbambe Mwamaso kupima uzito kesho mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/02/dulla-mbambe-mwamaso-kupima-uzito-kesho.html
0 Response to "Dulla Mbambe Mwamaso kupima uzito kesho"
Post a Comment