Loading...
title : RAIS WA ZIMBAMBWE KUWASILI NCHINI KESHO
link : RAIS WA ZIMBAMBWE KUWASILI NCHINI KESHO
RAIS WA ZIMBAMBWE KUWASILI NCHINI KESHO
Na Leandra Gabriel, Blogu ya jamii
RAIS wa awamu ya tatu wa Zimbabwe Emerson Mnangagwa anataraji kuwasili nchini mapema kesho kwa ziara ya siku mbili kuanzia June 28 hadi 29 mwaka huu.
Akizungumza na vyombo vya habari leo jijini Dar es salaam Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam Paul Makonda ameeleza kuwa Mnangagwa atapokelewa katika uwanja wa kimataifa wa mwalimu Nyerere na mwenyeji wake Rais John Magufuli majira ya saa tano kamili asubuhi.
Aidha ameeleza kuwa ujio huo wa Rais wa Zimbabwe una lengo kuu ambalo ni kudumumisha ushirikiano wa muda mrefu uliopo baina ya Tanzania na Zimbabwe tangu wakati wa kupigania uhuru wa taifa hili la kusini mwa Afrika.
Makonda amesema kwamba Mnangagwa ataondoka nchini june 29 asubuhi akisindikizwa na mwenyeji wake Rais Magufuli na ametoa wito kwa wakazi wa Dar es salaam kumkaribisha mgeni na wageni wote waingiao nchini kwa kuwafanya wajisikie wako nyumbani kwa muda wote watakaokuwa jijini.
Ikumbukwe kuwa hii ni ziara ya kwanza ya Rais Mnangagwa wa Zimbabwe kufika nchini Tanzania tangu alipoingia madarakani Novemba 2017.
Waandishi wa habari wakimsikiliza Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda.(Picha na Emmanuel Massaka Globu ya jamii)
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam,Paul Makonda akizungumza na waandishi wa habari leo kuhusu ziara ya kikazi ya Rais wa Zimbabwe Mh. Emerson Mnangagwa.(picha na Emmanuel Massaka wa Globu ya jamii)
Hivyo makala RAIS WA ZIMBAMBWE KUWASILI NCHINI KESHO
yaani makala yote RAIS WA ZIMBAMBWE KUWASILI NCHINI KESHO Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala RAIS WA ZIMBAMBWE KUWASILI NCHINI KESHO mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/06/rais-wa-zimbambwe-kuwasili-nchini-kesho.html
0 Response to "RAIS WA ZIMBAMBWE KUWASILI NCHINI KESHO"
Post a Comment