Loading...
title : MREMA AMGEUKIA MORA WAKE
link : MREMA AMGEUKIA MORA WAKE
MREMA AMGEUKIA MORA WAKE
Na Noel Rukanuga
Mwenyekiti wa Bodi ya Parole na Chama cha TLP Taifa Augustino Lyatonga Mrema ameamua kutumia muda wake kumtumika mungu na watanzania jambo ambalo naamini itakuwa chachu ya maendeleo kwa taifa.
Akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam, Mhe Mrema amesema kuwa uamuzi huo umeuchukua baada kupoma ugonjwa wa kasa ya mapafu ambao ulikuwa unamsumbua kwa muda mrefu.
Amesema kuwa baada ya kupona ugonjwa huo sasa ameamua kutumia muda wake wote kumtumia mungu na watanzania ili kuhakikisha katika viongozi waovu wote wanachukuliwa hatua kali za kisheria.
Mrema amesema kuwa katika nchi hii bado kuna viongozi waovu ambao wamekuwa wakifanya kazi zao kinyume na sheria na kusababisha baadhi ya watu wanaonewa.
"Kwenye nchi hii bado kuna maovu mengi sana, kwani watu wengi wamekuwa wakibambikiziwa kesi na kupelekwa mahakamani" amesema Mrema.
Amesema kuwa kama watu wengi wanalia ambao wapo gerezani na vituo vya polisi kutokana na kubambukiziwa kesi.
Katika hatua nyengine amempongeza Waziri wa Mambo ya ndani Kangi Lugola kwa kazi nzuri ambayo ameanza kuifanya hasa katika kupiga vita rushwa.
Amesema kuwa yupo tayari kumsaidia waziri wa mambo ya ndani kutokana kuna mambo mengi anayajua kwani aliwai kuwa waziri katika wizara hiyo.
"Rais wetu Mhe. Dkt.John Pombe Magufuli anapaswa kusaidiwa ili kuhakikisha nchi inakuwa safi" amesema Mrema.
Hivyo makala MREMA AMGEUKIA MORA WAKE
yaani makala yote MREMA AMGEUKIA MORA WAKE Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MREMA AMGEUKIA MORA WAKE mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/07/mrema-amgeukia-mora-wake.html

0 Response to "MREMA AMGEUKIA MORA WAKE"
Post a Comment