Loading...

Wafanyakazi 54 wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Watunukiwa vyeti vya ufanyakazi bora

Loading...
Wafanyakazi 54 wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Watunukiwa vyeti vya ufanyakazi bora - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Wafanyakazi 54 wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Watunukiwa vyeti vya ufanyakazi bora, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Wafanyakazi 54 wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Watunukiwa vyeti vya ufanyakazi bora
link : Wafanyakazi 54 wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Watunukiwa vyeti vya ufanyakazi bora

soma pia


Wafanyakazi 54 wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Watunukiwa vyeti vya ufanyakazi bora

Wafanyakazi wa Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) wamesisitizwa kufanya kazi kwa bidii , na kuzingatia nidhamu katika utendaji wao ili kutoa huduma bora na yenye viwango vya juu.
Kauli hiyo imetolewa leo jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa MNH Prof. Lawrence Museru alipokuwa akizungumza katika hafla fupi ya kuwatunuku Vyeti  wafanyakazi bora 54 wa Hospitali hiyo kwa mwaka 2018.
Akizungumza katika hafla hiyo  iliyoandaliwa kwa ajili ya kuwatunuku vyeti wafanyakazi hao, amesema serikali inathamini mchango wa kila mmoja katika kuhudumia Umma hivyo wafanyakzi wote hawana budi kutoa huduma bora na kufanya kazi kwa bidii bila kusukumwa.
‘’Nawapongeza kwakutoa huduma bora katika hospitali yetu naomba muendelee kuwa mabalozi wazuri , kwani mmekuwa mfano mzuri katika utekelezaji wa majukumu yenu ikiwa ni pamoja na utunzaji wa vifaa na kutoa lugha nzuri wakati wa kuwahudumiwa wateja’’. Amesema Prof. Museru.
Awali akikaribisha Mkurugenzi Mtendaji wa MNH, Mkurugenzi wa Rasilimali watu na utawala Bwn. Makwaia Makani amesema wafanyakazi bora 54 hao wamewakilisha Idara mbalimbali, majengo  na vitengo vya hospitali hiyo.
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili(MNH) Prof. Lawrence Museru (Katikati) akizungumza na baadhi ya watumishi wa MNH katika hafla fupi ya kuwatunuku vyeti wafanyakazi bora  wa hospitali hiyo. Kulia ni Mkurugenzi wa Rasilimali watu na utawala Bwn. Makwaia Makani, kushoto ni Mwenyekiti wa chama cha wafanyakazi Bwan. Mziwanda Salum na anayefuatia ni Afisa Utumishi Bwn. Michael Ngowi.
 Prof: Museru akimkabidhi cheti cha ufanyakazi bora Theophil Joseph

 Mmoja wa wafanyakazi bora Muuguzi Msaidizi Bi. Mkatareto Akyoo  akipokea cheti kutoka kwa Mkurugenzi Mtendaji Prof. Museru.
 Mfanyakazi bora kwa mwaka 2018 Philip Simya akikabidhiwa cheti mapema leo .
Wafanyakazi bora wakiwa katika picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji wa hospitali hiyo Prof; Lawrence Museru.


Hivyo makala Wafanyakazi 54 wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Watunukiwa vyeti vya ufanyakazi bora

yaani makala yote Wafanyakazi 54 wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Watunukiwa vyeti vya ufanyakazi bora Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Wafanyakazi 54 wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Watunukiwa vyeti vya ufanyakazi bora mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/08/wafanyakazi-54-wa-hospitali-ya-taifa.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Wafanyakazi 54 wa Hospitali ya Taifa Muhimbili Watunukiwa vyeti vya ufanyakazi bora"

Post a Comment

Loading...