Loading...

Dk.Kigwangalla ateta na Mjukuu wa Malkia wa Uingereza, Prince William Dar

Loading...
Dk.Kigwangalla ateta na Mjukuu wa Malkia wa Uingereza, Prince William Dar - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Dk.Kigwangalla ateta na Mjukuu wa Malkia wa Uingereza, Prince William Dar, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Dk.Kigwangalla ateta na Mjukuu wa Malkia wa Uingereza, Prince William Dar
link : Dk.Kigwangalla ateta na Mjukuu wa Malkia wa Uingereza, Prince William Dar

soma pia


Dk.Kigwangalla ateta na Mjukuu wa Malkia wa Uingereza, Prince William Dar

 Mjukuu  wa Malkia wa Uingereza, Prince William (katikati) akiteta jambo na Waziri wa Maliasili na Utalii Dkt. Hamisi Kigwangalla (kushoto) wakati  alipowasili kwenye ofisi ndogo ya wizara hiyo Jijini Dar es Salaam. Kulia ni Waziri wa Sheria na Katiba, Mhe. Profesa Paramagamba Kabudi.



Waziri wa Maliasili na Utalii, Dkt. Hamisi Kigwangalla jana amekutana na kuzungumza na Mjukuu  wa Malkia wa 
Uingereza, Prince William ambaye yupo nchini kwa ziara ya 
siku tatu.

Prince William ambaye aliwasili nchini Septemba 26, 2018 
kwa ziara maalum ambapo awali alikutana na Rais wa 
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ikulu ya Magogoni Jijini 
Dar es Salaam, Mhe. Dkt. John Pombe Joseph Magufuli na 
baadae kupokelewa ofisini kwa Waziri w Maliasili na Utalii, 
Dkt. Hamisi Kigwangalla, amesema kuwa amefurahia uwepo 
wake hapa nchini hali iliyopelekea kukaa kwa muda huo 
tofauti na Nchi zingine ambazo amekaa kwa siku moja.

Prince William ameweza kumtembelea Dk. Kigwangalla 
katika ofisi ndogo ya Wizara hiyo Jijijini Dar es Salaam, 
ambapo katika mazungumzo baina ya wawili hao, ikiwemo 
suala la kuomba msaada wa kusaidia Sekta ya Utalii.

“Kiukweli tokea kumpokea hapa Nchini alipoingia Septemba 
26, Prince William amefurahia ..na nimeweza 
kumuomba  msaada wa masuala mbalimbali ya kusaidia 
Sekta ya Utalii na Uhifadhi wa Nchi yetu kutokana na 
yeye  kuwa na mapenzi ya kipekee kwenye uhifadhi na pia 
anakumbukumbu nzuri na Tanzania kiasi cha kukaa siku 
tatuhapa tofauti na nchi zingine alizokaa siku moja” 
ameeleza Dkt. Kigwangalla.

Miongoni mwa mambo Waziri Dkt. Kigwangalla aliomba 
asaidiwe na Prince William ni pamoja na suala la kukijengea 
uwezo kikosi kazi cha kudhibiti ujangili Nchini hii ni 
pamojana kusaidia kwenye masuala ya utalaam, zana za 
kisasa za kiintelijensia na mafunzo.

Pia Dkt. Kigwangalla alimuomba Prince William kusaidia 
kwenye mradi wa kujenga makumbusho tatu za 
kuhifadhi  meno ya tembo ambapo Wizara inakusudio la 
kujenga makumbusho hayo katika Mikoa ya Dodoma, 
Arusha na Dar es Salaam.

“lengo la kumuomba atusaidie katika kujenga makumbusho 
ya kuhifadhi meno ya tembo ni kutokana na Tanzania kuwa 
miongoni mwa nchi za awali tano za Afrika kusaini mpango 
wa kulinda tembo kule nchini uingereza mwaka 2008.

Ambapo katika progam hiyo, nchi zote ambazo zimesaini, 
zinajifunga kwa kufanya meno hayo ya tembo yasiweze 
kutumika tena kibiashara na kiuchumi kwa maana ya 
kwamba meno hayo hayawezi kuuzwa tena kwa faida za 
kiuchumi hivyo na sisi tumeamua kuyalinda na kuyahifadhi 
ili iwe ukumbusho vizazi na vizazi tofauti na nchi zingine 
ambazo wao waliamua kuziteketeza kwa kuzichoma moto” 
alieleza Dkt. Kigwangalla.

Aidha, Dkt. Kigwangalla alimuomba Prince William msaada 
mwingine wa ndege aina ya Helkopta Nne, ikiwemo mbili 
zitakazokuwa  kwa ajili ya dharura na mbili zingine kwa ajili 
ya doria kwenye baadhi ya maeneo  ya uhifadhi nchini.

Prince William na ujumbe wake huo umeweza kutembelea 
Hifadhi ya Taifa ya Mkomazi na pia Chuo cha Wanyamapori 
cha Mweka (College of African Wildlife Management, Mweka 
(CAWM), kilichopo Moshi, mkoani Kilimanjaro na baada ya 
hapo ataendelea na ziara yake Nchini Kenya.

Lengo kuu la ziara hiyo ya Prince William ni pamoja na 
kufuatilia juhudi za kukabiliana na ujangili na uhifadhi wa 
wanyama ikiwemo tembo.


Hivyo makala Dk.Kigwangalla ateta na Mjukuu wa Malkia wa Uingereza, Prince William Dar

yaani makala yote Dk.Kigwangalla ateta na Mjukuu wa Malkia wa Uingereza, Prince William Dar Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Dk.Kigwangalla ateta na Mjukuu wa Malkia wa Uingereza, Prince William Dar mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/09/dkkigwangalla-ateta-na-mjukuu-wa-malkia.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Dk.Kigwangalla ateta na Mjukuu wa Malkia wa Uingereza, Prince William Dar"

Post a Comment

Loading...