Loading...
title : KUMBUKUMBU YA MIAKA MITANO YA MAMA FORTUNATA JOSEPH MSOKA
link : KUMBUKUMBU YA MIAKA MITANO YA MAMA FORTUNATA JOSEPH MSOKA
KUMBUKUMBU YA MIAKA MITANO YA MAMA FORTUNATA JOSEPH MSOKA
MPAKA TUTAKAPOKUTANA TENA KWENYE MAHALI PENYE ENZI NA UTUKUFU

Mama Fortunata Joseph Msoka; tunakumbuka muda wote tulipokuwa nawe tukifurahi pamoja. Tunatamani Mungu angetupa upendeleo ukarudi hata kwa muda tu tukakaa na kuzungumza kama ulivyokuwa ukifanya; ukitufundisha mema, kushika Imani na kuwapenda ndugu na marafiki.
Kwa hakika ulikuwa mtu pekee sana katika maisha yetu sisi watoto wako.
Ni miaka mitano sasa lakini bado hatujaamini kweli umeondoka kwenye maisha yetu. Kila tukikuita hauitiki, tukija nyumbani haupo; ni ukweli ambao ni mchungu kumeza na maumivu yasiyoisha. Daima utadumu kwenye mioyo yetu watoto wako Paul na Constatine Msoka, Jackiline na Rose Mdami.
Wajukuu wamekosa wa kumtania wamebaki kulibeba jina lako kwenye nyoyo zao. Hakika upendo wako hauta sahaulika kwa watu wote ulioshi nao; majirani, marafiki, WAWATA Parokia ya Ukonga na wanafunzi wako.
Tunasema Buriani uendelee kulala usingizi wa Amani na Mungu Mwenyezi akaitulize roho yako na ya Baba yetu mahali pema Mbingun - Amina
Ufunuo 21:4 “ naye atafuta kila chozi katika macho yao wala mauti haitakuwapo tena, wala maombolezo, wala kilio, wala maumivu hayatakuwepo tena, kwakuwa mambo ya kwanza yamekwisha kupita”
Hivyo makala KUMBUKUMBU YA MIAKA MITANO YA MAMA FORTUNATA JOSEPH MSOKA
yaani makala yote KUMBUKUMBU YA MIAKA MITANO YA MAMA FORTUNATA JOSEPH MSOKA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala KUMBUKUMBU YA MIAKA MITANO YA MAMA FORTUNATA JOSEPH MSOKA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/09/kumbukumbu-ya-miaka-mitano-ya-mama.html
0 Response to "KUMBUKUMBU YA MIAKA MITANO YA MAMA FORTUNATA JOSEPH MSOKA"
Post a Comment