Loading...

MAHAKIMU MBULU, WAKUMBUSHWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KIKAMILIFU

Loading...
MAHAKIMU MBULU, WAKUMBUSHWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KIKAMILIFU - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa MAHAKIMU MBULU, WAKUMBUSHWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KIKAMILIFU, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : MAHAKIMU MBULU, WAKUMBUSHWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KIKAMILIFU
link : MAHAKIMU MBULU, WAKUMBUSHWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KIKAMILIFU

soma pia


MAHAKIMU MBULU, WAKUMBUSHWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KIKAMILIFU

Na Catherine Francis, Mahakama Kuu - Arusha

Jaji Mfawidhi, Mahakama Kuu- Kanda ya Arusha, Mhe. Mosses Mzuna, amewakumbusha Mahakimu kutekeleza wajibu wao ipasavyo ili kuhakikisha haki inatendeka kwa kila mwananchi na kwa wakati.

Akiwa ziarani Mahakama ya Wilaya Mbulu, Mhe. Jaji Mzuna aliwakumbusha Mahakimu wilayani humo kuwa wanapaswa kutoa adhabu kwa kuzingatia ukubwa wa kosa lenyewe na si kwa kuhamasishwa na hisia juu ya kesi husika. “Wajibu wa kila Hakimu ni kuhakikisha haki inatendeka na kupitia mwenendo wa shauri na maamuzi yaliyotolewa kabla hawajaruhusu jalada kwenda kwenye ngazi nyingine za Mahakama,” alisistiza Mhe. Mzuna.

Aidha; Mhe. Jaji Mfawidhi alisisitiza juu ya umuhimu wa taarifa za mashauri kufikia wadaawa kwa wakati unaostahili ambapo mwenendo wa shauri pamoja na nakala ya hukumu vinatakiwa viwafikie wadaawa kwa wakati. Mhe. Mzuna alisema endapo taarifa hizi zitawafikia Wadaawa mapema zinawawezesha kufanya hatua nyingine kama watakuwa hawajaridhishwa na maamuzi ya Mahakama hiyo.

Katika kusititiza hilo Mheshimiwa Jaji Mzuna alifanya ukaguzi mdogo wa majalada ya mashauri yaliyokamilika ili kuweza kugundua ni kwa jinsi gani Mahakimu wamekuwa wakitekeleza wajibu wao.

Ukaguzi huo ulihusisha majalada ya Mahakama ya Wilaya Mbulu na majalada ya Mahakama ya mwanzo Endagikot. Pia aliwapa maelekezo na mapendekezo pale alipogundua kuna changamoto katika kutekeleza wajibu wao.

Katika ziara hiyo, Mhe. Jaji Mfawidhi alikutana pia na Wazee wa Baraza wa Wilaya ya Mbulu ili kuweza kuwafahamu na kujua changamoto wanazokabiliana nazo ambazo zinakwamisha ufanisi wa kazi zao.
Jaji Mzuna akikagua majalada ya Mahakama ya mwanzo ya Endagikot wilayani Mbulu.


Hivyo makala MAHAKIMU MBULU, WAKUMBUSHWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KIKAMILIFU

yaani makala yote MAHAKIMU MBULU, WAKUMBUSHWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KIKAMILIFU Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala MAHAKIMU MBULU, WAKUMBUSHWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KIKAMILIFU mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/10/mahakimu-mbulu-wakumbushwa-kutekeleza.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "MAHAKIMU MBULU, WAKUMBUSHWA KUTEKELEZA MAJUKUMU YAO KIKAMILIFU"

Post a Comment

Loading...