Loading...
title : MPINA AWATAKA VIONGOZI WOTE WA SERIKALI KUSHIRIKI KIKAMILIFU KWENYE ULINZI WA RASLIMALI ZA MIFUGO
link : MPINA AWATAKA VIONGOZI WOTE WA SERIKALI KUSHIRIKI KIKAMILIFU KWENYE ULINZI WA RASLIMALI ZA MIFUGO
MPINA AWATAKA VIONGOZI WOTE WA SERIKALI KUSHIRIKI KIKAMILIFU KWENYE ULINZI WA RASLIMALI ZA MIFUGO
NA JOHN MAPEPELE, MARA
WAZIRI wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina amewataka viongozi wote wa serikali kuanzia ngazi za vijiji,wilaya kushiriki kikamilifu katika ulinzi wa rasilimali za mifugo badala ya hali ilivyo sasa ya kuiacha ikitoroshwa kwenda nchi za nje kwa kuamini kwamba jukumu la ulinzi wa rasilimali hizo ni la Wizara ya Mifugo na Uvuvi peke yake na ikosesha serikali mapato.
Waziri Mpina ameyasema hayo wakati akizundua mnada wa mpakani wa Kimataifa wa Mifugo katika eneo la Kirumi Wilayani Butiama mkoani Mara ambapo ameagiza kufungwa kwa minada yote ya mifugo iliyofunguliwa kinyemela kwani imekuwa kichocheo cha upotevu wa mapato wa Serikali na kuonya wanaoanzisha minada hiyo bila kufuata taratibu zilizopo watachukuliwa hatua kali kwa mujibu wa sheria.
Aidha amemuagiza Katibu Mkuu Mifugo, Profesa Elisante Ole Gabriel kuanza mara kuihakiki minada yote iliyopo nchini ili kuibaini ambayo imeanzishwa kinyume cha sheria iweze kufutwa.“wako watu wanafungua minada kila sehemu wanaamua tu wakati taratibu za ufunguzi wa minada wanazijua kabisa ya kwamba ni lazima wizara iridhie kufunguliwa kwa mnada huo”alisisitiza Waziri Mpina
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akikata utepe kufungua Mnada wa Kimataifa wa Mifugo Kirumi ulioko wilayani Butiama mkoani Mara juzi, wengine wanaoshuhudia ni Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima{kushoto},Mkuu wa Wilaya ya Butiama, Annarose Nyamubi}kulia} na Katibu Mkuu Mifugo, Profesa Elisante Ole Gabriel.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina akifunua kitambaa katika jiwe la msingi la ufunguzi wa Mnada wa Kimataifa wa Mifugo Kirumi ulioko wilayani Butiama mkoani Mara juzi, wengine wanaoshuhudia ni Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima{kulia} na Katibu Mkuu Mifugo, Profesa Elisante Ole Gabriel }kushoto}.
Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina aliyenyanyua mkono akiwa na Katibu Mkuu Mifugo, Profesa Elisante Ole Gabriel (kulia kwake) wakati wa ufunguzi wa Mnada wa Kimataifa wa Mifugo Kirumi ulioko wilayani Butiama mkoani Mara juzi.
Hivyo makala MPINA AWATAKA VIONGOZI WOTE WA SERIKALI KUSHIRIKI KIKAMILIFU KWENYE ULINZI WA RASLIMALI ZA MIFUGO
yaani makala yote MPINA AWATAKA VIONGOZI WOTE WA SERIKALI KUSHIRIKI KIKAMILIFU KWENYE ULINZI WA RASLIMALI ZA MIFUGO Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala MPINA AWATAKA VIONGOZI WOTE WA SERIKALI KUSHIRIKI KIKAMILIFU KWENYE ULINZI WA RASLIMALI ZA MIFUGO mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/10/mpina-awataka-viongozi-wote-wa-serikali_18.html
0 Response to "MPINA AWATAKA VIONGOZI WOTE WA SERIKALI KUSHIRIKI KIKAMILIFU KWENYE ULINZI WA RASLIMALI ZA MIFUGO"
Post a Comment