Loading...

Mtoto aliouawa kwa kipigo cha mama yake azikwa na mamia Babati

Loading...
Mtoto aliouawa kwa kipigo cha mama yake azikwa na mamia Babati - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Mtoto aliouawa kwa kipigo cha mama yake azikwa na mamia Babati, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Mtoto aliouawa kwa kipigo cha mama yake azikwa na mamia Babati
link : Mtoto aliouawa kwa kipigo cha mama yake azikwa na mamia Babati

soma pia


Mtoto aliouawa kwa kipigo cha mama yake azikwa na mamia Babati



Na John Walter,BABATI

JESHI la Polisi Mkoani Manyara  linamshikilia Mariamu Daudi [40] mkazi wa wa mtaa wa Komoto Babati mjini  kwa tuhuma za kumuua mtoto wake  Emmanuel Justine [11] mwanafunzi wa  darasa la tatu katika shule ya msingi Kwang’w huku likimsaka  kijana mmoja  aliyefahamika kwa jina la Amani ambaye alishirikiana na mama huyo.

Akizungumza 
  kamanda wa polisi mkoani hapa Augustino Senga  alithibitisha  kutokea kwa tukio hilo  na mpaka sasa  wanamshikilia  mama mzazi wa mtoto huyo kwa mahojiano zaidi.

Aidha kamanda Senga  alisema  mtoto huyo alidaiwa kuiba nyiwa  kwa Aman  ambaye anasakwa na polisi na mtuhumiwa anayesakwa  alimshambulia  mwanafunzi huyo  kwa kumpiga fimbo huku akiwa amesimamiwa na mama yake mzazi wa mtoto aliyeuliwa.

“Taarifa tulizopata kijana aliyefanya  unyama huo anajulikana  mitaani  hivyo tunaendelea kufanya upelelezi   na tukimkamata hatua zingine zitaendelea  za kuwafikisha  watuhumiwa mahakamani kwa ajili ya kujibu mashtaka,’’Alisema Senga

 Alitumia fursa hiyo kuitaka jamii kuwalea watoto katika maadili mazuri  na kuepuka kutoa adhabu  ambazo zimezidi kipimo kwa watoto  kwa kua kufanya hivyo ni kuvunja  sheria  za nchi  na wanaokiuka  serikali lazima iwachukulie hatua.

Mmoja wa majirani  waliosaidia kumnusuru mtoto huyo Stela Michael alisema  mama yake  aliwaambia mtoto huyo amezidi utukutu  hivyo amechoka  kuletewa mashitaka  nyumbani kwake  lakini anasema  mama huyo adhabu  aliyompa mtoto ilipitiliza kuzidi uwezo.

“Mimi niliitwa na mtoto mwenzake aliyedaiwa kua walichapwa pamoja akisema Emma ananiita baada ya kufika nilimkuta mtoto anagalagala chini ameishiwa na nguvu  na mama yake akaja tukasaidiana kumpa uji aliposikia mama yake aligoma kunywa  lakini nilipomnywesha mimi na akasikia sauti yangu alikubali akanywa mara moja na  kuishiwa nguvu ndio walimpeleka Hospitali,’’Alisema jirani huyo.

Naye mwenyekiti wa mtaa wa Komoto  Paschal Hondi  alisema matukio ya ukatili  katika mtaa huo yamekuwa ni endelevu na baba yake na mtoto huyo alisema marehemu amekufa ghafla  nay eye anadai hakuwepo nyumbani wakati mauti yanamkuta mwanae.

Aliongeza kua msiba huo wao wameupokea kwa masikitiko makubwa  maana umeigusa jamii  na matukio  ya namna hiyo ya kikatili yanaendelea kujitokeza katika mtaa huo licha ya serikali kupiga  kelele dhidi ya ukatili.

Kwa upande wake  Justine Mkilanyi  ambaye ni baba wa mtoto aliyeuwawa  alisema mtoto wake alienda shuleni  siku ya ijumaa akiwa mzima  na baadaye alirejea na kusema kua walimu wamemrudisha nyumbani kua  aende na  baba yake shuleni jambo ambalo  Mkilanyi akuridhia maana alikua anawahi kazini na akamuambia aende na mama yake.

“Ndipo walienda na mama yake na akaambiwa na walimu kua mtoto wake ni mtukutu ambapo  waliulizwa  wanafunzi wa darasani  kwake kua nani aliwahi kupigwa na Emmanuel ndio darasa  zima  liliamka,’’Alisema Mkilanyi.

Alifafanua kua  mke wake aliambiwa arudi nyumbani na mtoto wake  na  aliporudi na mtoto huyo walimkuta baba huyo bado yupo nyumbani  na mtoto wake alimwambia kua amefukuzwa na alimlalamikia  kuwa alishamwambia  amuhamishe shule hiyo toka yuko darasa la kwanza  kumpeleka  shule ya binafsi.

 “Mimi nilimuomba  avumilie  nije nimpeleke  shule hiyo nitakua ninalipa kidogo kidogo ila aliniambia baba  ninaondoka sasa  ndipo nikaenda kazini niliporudi jioni sikumkuta nikamtafuta  mpaka saa nne usiku sikumpata  kesho yake nikapata taarifa alilala kwa ndugu yangu,’’Alisema Mkilanyi

Aidha alisema  kesho yake alipoenda kazini  kurudi nyumbani alikuta mauti yamemkuta  na watu wamejaa  nyumbani kwake, wakati huo aliiambia Nipashe kua huyo mtoto ndio alimpenda sana maana alikkua anaweza kufanya kazi za ufundi, ufugaji  na uchoraji kama baba yake  ambaye anaona angemrithi.

 Kituo hiki  kilizungumza na  mwalimu  wa darasa wa mwanafunzi huyo Emmanuel  na kumuuliza kama kweli  mtoto huyo walimshindwa walimu  na kumrudisha nyumbani kwa muda usiojulikana  lakini  mwalimu Nuru Belshaza  alikana kumrudisha nyumbani mwanafunzi huyo huku akisema wao hawawezi kumshindwa mwanafunzi.

Katika hali ya kusikitisha juu ya tukio hilo mashuhuda wengi waliozungumza  kwa sharti la kutokuandikwa walisema  mama wa mtoto huyo  alishirikiana na  Amani  kumcharaza  kwa kutumia fimbo ya mbaazi huku mama yake akitumia mpini na wengine wakidai walimfunga mikono na miguu na kuanza kumtembezea kichapo bila huruma  licha ya mwanafunzi huyo kupiga kelele  kuomba msamaha.

Wengine waliongeza kuwa  mama  huyo alimlipatia  shilingi elfu kumi [10,000] ili kijana huyo amsaidie kumkimbiza mtoto huyo na  waweze kumpa adhabu  ili abadilike  maana alikuwa ni kero nyumbani na mitaani kwa baadhi ya watu.

 Mwinjilisti  Raymond  Francis aliyeendesha ibada ya mazishi ya mwanafunzi huyo aliwaambia waombolezaji kuwa  tukio hilo ni la kinyama  hivyo wawe  wanatoa adhabu  yenye kipimo ambayo haitageuka kuwa chukizo kwa Mungu maana inaweza  kumfanya mtoa adhabu aonekane  ametoa hukumu wakati kazi ya hukumu ni ya Mungu peke yake.


Hivyo makala Mtoto aliouawa kwa kipigo cha mama yake azikwa na mamia Babati

yaani makala yote Mtoto aliouawa kwa kipigo cha mama yake azikwa na mamia Babati Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Mtoto aliouawa kwa kipigo cha mama yake azikwa na mamia Babati mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/11/mtoto-aliouawa-kwa-kipigo-cha-mama-yake.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Mtoto aliouawa kwa kipigo cha mama yake azikwa na mamia Babati"

Post a Comment

Loading...