Loading...
title : Mikataba ya wakandarasi wa umeme vijijini kupitiwa na wanasheria wa Serikali
link : Mikataba ya wakandarasi wa umeme vijijini kupitiwa na wanasheria wa Serikali
Mikataba ya wakandarasi wa umeme vijijini kupitiwa na wanasheria wa Serikali
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu ameeleza kuwa, Wanasheria wa Wizara ya Nishati, Wakala wa Nishati Vijijini (REA) na Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) wataanza kupitia mikataba ya wakandarasi wanaosambaza umeme vijijini ili kuchukua hatua za kuwawajibisha wakandarasi wanaotekeleza miradi hiyo kwa kusuasua.
Aliyasema hayo jijini Dodoma wakati wa kikao chake na Mameneja wa TANESCO wa Kanda, Mikoa, Wilaya na wasimamizi wa miradi ya usambazaji umeme vijijini kutoka Wizara ya Nishati, REA na TANESCO.
“ Yako baadhi ya maeneo ambayo Wakandarasi hawafanyi vizuri kama vile Mtwara, Arusha, Kilimanjaro, Manyara, Morogoro, Shinyanga, Singida, Tabora (Kaliua, Uyui, Urambo), Dodoma na Tanga (Wilaya ya Korogwe, Mkinga na Pangani), ambao utekelezaji wao katika mradi wa usambazaji umeme wa Awamu ya Tatu, mzunguko wa kwanza, wako chini ya asilimia 20,” alisema Mgalu.
Naibu Waziri alitoa agizo kuwa, wakandarasi katika maeneo hayo wahakikishe kuwa, wanafanya kazi kwa kasi na ufanisi ikiwemo kuweka magenge mengi ya kazi, uwepo vifaa na wasimamizi wa miradi wa kutosha ili kuepuka kuchukuliwa hatua za kisheria na Serikali na pia kutorudisha nyuma juhudi za Serikali za kusambaza umeme vijijini.
Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (katikati), akimsikiliza Mwakilishi wa Kaimu Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati, Haji Janabi wakati wa kikao kazi na watendaji wa REA na TANESCO na wasimamizi wa miradi ya usambazaji umeme vijijini kutoka REA, TANESCO na Wizara ya Nishati. Wengine katika picha ni Kamishna Msaidizi wa Nishati Jadidifu, Edward Ishengoma (wa kwanza kushoto), Mkurugenzi Mtendaji wa TANESCO, Dkt Tito Mwinuka (wa pili kulia) na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa REA, Mhandisi Amos Maganga (wa kwanza kulia).
Baadhi ya watendaji wa REA na TANESCO na wasimamizi wa miradi ya usambazaji umeme vijijini kutoka REA, TANESCO na Wizara ya Nishati wakimsikiliza Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (hayupo pichani) wakati wa kikao kazi kilichofanyika jijini Dodoma.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Hivyo makala Mikataba ya wakandarasi wa umeme vijijini kupitiwa na wanasheria wa Serikali
yaani makala yote Mikataba ya wakandarasi wa umeme vijijini kupitiwa na wanasheria wa Serikali Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Mikataba ya wakandarasi wa umeme vijijini kupitiwa na wanasheria wa Serikali mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/12/mikataba-ya-wakandarasi-wa-umeme.html
0 Response to "Mikataba ya wakandarasi wa umeme vijijini kupitiwa na wanasheria wa Serikali"
Post a Comment