Loading...

Halmashauri ya Kilolo yakopesha wanawake navijana Tsh milioni 110

Loading...
Halmashauri ya Kilolo yakopesha wanawake navijana Tsh milioni 110 - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Halmashauri ya Kilolo yakopesha wanawake navijana Tsh milioni 110, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Halmashauri ya Kilolo yakopesha wanawake navijana Tsh milioni 110
link : Halmashauri ya Kilolo yakopesha wanawake navijana Tsh milioni 110

soma pia


Halmashauri ya Kilolo yakopesha wanawake navijana Tsh milioni 110

NA  FRANCIS GODWIN,IRINGA 

KATIKA utekelezaji wa agizo la  serikali la  kila Halmashauri  nchini  kutenga kiasi cha fedha asilimia 10 ya makusanyo yake ya ndani kwa ajili ya  kuyawezesha makundi ya  vijana ,walemavu na wanawake ,Halmashauri ya wilaya ya Kilolo mkoani Iringa   imetumia sherehe  za siku ya  wanawake duniani kwa kutoa  mikopo kiasi cha shilingi milioni 110 kwa vikundi  mbali mbali  vikiwemo  vikundi vya wanawake katika wilaya  hiyo.

Akizungumza kwa niaba ya mkurugenzi  wa Halmashauri ya Kilolo Aloyce Kwezi mwakilishi  wake katika sherehe hizo juzi  Dr John Mwingira alisema  kuwa  kwa kutambua  umuhimu wavikundi vya wanawake  wajasiliamali ndani ya  wilaya ya  Kilolo Halmashauri  iliona ni vizuri  kuweza kutumia  siku hiyo ya wanawake duniani inayoadhimishwa Machi 8 kote  duniani kwa ajili ya  kuwawezesha  wanawake hao kiuchumi.

Kuwa  mikopo hiyo ambayo imetolewa kwa wanawake ni mikopo isiyo na riba na  wakopaji watatakiwa kurejesha  mikopo  hiyo kwa muda uliopangwa bila ya kutozwa  riba yoyote na  kuwa pindi mikopo hiyo inaporejeshwa kwawakati vikundi vingine vya  wanawake huendelea  kukopeshwa zaidi  .

" Halmashauri  kupitia makusanyo ya mapato ya  ndani  imeendelea kutekeleza agizpo la  serikali lililotolewa na Rais Dkt John Magufuli kwa Halmashauri zote nchini kupitia makusanyo  yake ya ndani kutenga asilimia 10 kwa  ajili ya  kuwakopesha vikundi vya wanawake ,walemavu na vijana na  halmashauri yetu  imekuwa ikitekeleza kwavitendo na kwa  wakati agizo hilo " alisema 

 Kuwakiasi hicho cha  shilingi milioni 110 kimetumika kukopesha wanawake ,vijana na walemavu ambao kwa  umoja  wao  walikabidhiwa  fedha hizo kupitia sherehe hizo za siku ya wanawake duniani na kuwa azma ya  Halmashauri kuendelea kuwasaidia mikopo vijana ,wanawake na  walemavu ambao  wamejiunga katika vikundi .

Alisema kuwa kupitia  sherehe hizo vikundi vya  wanawake 59 kutoka kata mbali mbali za  wilaya ya Kilolo walikopeshwa  kiasi cha  shilingi milioni 66 wakati  vikundi vya  vijana  vilivyopewa mkopo ni vikundi  24 ambavyo vilikopeshwa  shilingi milioni 43 na kikundi kimoja  cha  walemavu kilichokopeshwa  kiasi cha  shilingi milioni 1.

Akikabidhi   mfano wa hundi ya  mikopo kwa vikundi hivyo   mwenyekiti wa Halmashauri ya  Kilolo  Vallence Kihwaga  alisema  kuwa  fedha  hizo za mikopo  walizokopeshwa na sehemu  tu ya bajeti  ya Halmashauri  iliyotengwa kwa mwaka 2019 na kuwa kwa sasa  wameanza kutekeleza  matumizi ya  bajreti hiyo kwa kuanza kutoa mikopo kwamakundi mbali mbali  na  wataendelea  kutoa  mikopo  na kuwataka  walengwa  kuendelea kujiunga katika vikundi mbalimbali vya ujasiliamali .

" Tutaendelea  kutoa mikopo  hii  mara kwa mara kama ambavyo bajeti yetu ilivyopangwa  kwa mwaka huu  na  tunauhakika kuwa baada ya leo kutoa  mikopo hii muda si mrefu  tutatoa mikopo tena kwa makundi ya  wanawake ,vijana na walemavu  hivyo  endeleeni  kuunda vikundi vyenye  tija  vya ujasiliamali nacha kujivunia ni tayari Rais wetu mpendwa Dkt  John Magufuli kwa  kuwajali  wajasilimali amekwisha  toa  vitambulisho kwa kila halmashauri kwa ajili yenu  wajasiliamali kazikwenu  kuchangamkia vitambulisho  hivyo ili msinyanyasike mnapofanya shughuli zenu" alisema Kihwaga.

Aidha  alisema wakopaji ambao watachelewesha  kurejesha mikopo ama  kushindwa kurejesha kabisa  watakuwa  wamejiondoa katika orodha ya  watakaoendelea  kukopeshwa mikopo hiyo na wale  watakaoonyesha uaminifu wataendelea  kunufaika na mikopo hiyo inayotengwa na Halmashauri ikiwa ni asilimia 4 vijana  na asilimia 2 walemavu huku wanawake wakipata nao asilimia 4  katika asilimia 10 ya mikopo itokanayo ya makusanyo ya ndani ya Halmashauri .

Kihwaga  alisema kuwa  sifa kuu ya vikundi  hivyo kukopeshwa ni kuwa kuwa na akaunti bank ambayo ni hai na sio akaunti iliyosinzia ambayo haionyeshi kama inatumika kuweka na kuchukua  fedha .

Kwa upande wake wake  wanawake    wanufaika na  mikopo  hiyo Amina Sanga akizungumzia mikopo hiyo alisema  kuwa  imekuwa ni  mkombozi mkubwa kwao kwani  itawawezesha kuongeza uzalishaji katika  kikundi na  kuwa pale  wanawake  wanapokuwa na kipato  kizuri ndani ya familia hata ndoa zao zimekuwa zisimama pasipo  kuyumba  kwani mama anakuwa na sauti  kama baba ndani ya nyumba.
 Mwenyekiti wa Halmashauri ya  wilaya ya Kilolo mkoani IringaVallence Kihwaga (mwenye koti jeusi kushoto) na mwakilishi wamkurugenzi wa Halmashauriya Kilolo Dr John Mwingira ( wapili kulia)  wakiwakabidhi  mfano wahundi ya shilingi milioni 110  wanawake wa vikundi 59 vya wajasiliamali wilaya ya Kilolo kwa  niaba ya vikundi vya walamavu na vijana  juzi  wakati wa sherehe za  wanawake wilaya ya Kilolo (picha na Francis Godwin). 
Mwenyekiti wa Halmashauri ya wilaya ya Kilolo mkoani Iringa Vallence Kihwaga (kushoto) akimkabidhi mmoja kati ya wazee wanaotoka katika familia masikini ndani ya mji wa Ilula kwa niaba ya wazee wengine ,msaada wa sabuni na vitu mbali mbalivilivyotolewa na wanawake wa wilaya ya Kilolo kwa wazee hao kwa ajili ya kusherekea siku ya wanmawake duniani juzi Machi 8 mwaka huu (Picha na Francis Godwin).


Hivyo makala Halmashauri ya Kilolo yakopesha wanawake navijana Tsh milioni 110

yaani makala yote Halmashauri ya Kilolo yakopesha wanawake navijana Tsh milioni 110 Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Halmashauri ya Kilolo yakopesha wanawake navijana Tsh milioni 110 mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2019/03/halmashauri-ya-kilolo-yakopesha.html

Subscribe to receive free email updates:

0 Response to "Halmashauri ya Kilolo yakopesha wanawake navijana Tsh milioni 110"

Post a Comment

Loading...