Loading...

WATU NANE WAPATA MAJERAHA KATIKA AJALI ILIYOTOKEA VIGWAZA

Loading...
WATU NANE WAPATA MAJERAHA KATIKA AJALI ILIYOTOKEA VIGWAZA - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa WATU NANE WAPATA MAJERAHA KATIKA AJALI ILIYOTOKEA VIGWAZA, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : WATU NANE WAPATA MAJERAHA KATIKA AJALI ILIYOTOKEA VIGWAZA
link : WATU NANE WAPATA MAJERAHA KATIKA AJALI ILIYOTOKEA VIGWAZA

soma pia


WATU NANE WAPATA MAJERAHA KATIKA AJALI ILIYOTOKEA VIGWAZA

NA MWAMVUA MWINYI, CHALINZE 

WATU nane wapata majeraha baada ya gari la abiria , mali ya kampuni ya Friends ikitokea Dar es salaam kuelekea Kampala nchini Uganda kupata ajali ,eneo la Kwazoka, kata ya Vigwaza, Chalinze mkoani Pwani. 

Aidha dereva wa gari hilo lenye namba za usajili, UAY 458 F aina ya Scania ,Bashiru Telu mkazi wa nchini Uganda amekimbia baada ya kutokea ajali hiyo. 

Kamanda wa polisi mkoani Pwani, ACP Wankyo Nyigesa, alithibitisha kutokea kwa ajali hiyo mchana march 18,mwaka huu na kusema gari hiyo ilikuwa na abiria 42.

Alieleza, gari hiyo iliacha njia na kupinduka na kusababisha majeruhi hao ambapo chanzo cha ajali ni dereva huyo kujaribu kuyapita magari mengine bila kuchukua tahadhari. 

Wankyo aliwataja waliopata majeraha kuwa ni Kubo Zuberi (24) aliyepata jeraha katika mkono wa kulia mkazi wa Uganda ,Rudigo Benjamin (24) na Aisha Salin (34) mkazi wa Dar es salaam ameumia kichwa.

Wengine ni Theonestina Gedioni (29) mkazi wa Tabata ,Baiga Jacquie (30) mkazi wa Uganda, Nasra Amani (12) mkazi wa Dar es salaam, Farouqs Natkunda (22)mkazi wa Uganda na Hassan Omary mkazi wa Mbezi Dar es salaam. 

"Majeruhi hao walikimbizwa katika kituo cha afya Mlandizi, ambapo wanaendelea na matibabu "alifafanua Wankyo. 

Kamanda huyo alitoa rai kwa madereva wa vyombo vya moto kutii sheria za usalama barabarani. 

Vile vile wasafiri wanaotumia vyombo hivyo kuendelea kuwafichua madereva wanaovunja sheria za usalama barabarani ili waweze kuchukuliwa hatua kwa kupiga namba za makamanda wa mkoa wa wakuu wa usalama barabarani.
Kamanda wa polisi mkoani Pwani, ACP Wankyo Nyigesa


Hivyo makala WATU NANE WAPATA MAJERAHA KATIKA AJALI ILIYOTOKEA VIGWAZA

yaani makala yote WATU NANE WAPATA MAJERAHA KATIKA AJALI ILIYOTOKEA VIGWAZA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala WATU NANE WAPATA MAJERAHA KATIKA AJALI ILIYOTOKEA VIGWAZA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2019/03/watu-nane-wapata-majeraha-katika-ajali.html

Subscribe to receive free email updates:

0 Response to "WATU NANE WAPATA MAJERAHA KATIKA AJALI ILIYOTOKEA VIGWAZA"

Post a Comment

Loading...