Loading...

Watakiwa kutoa taarifa za tukio lenye shaka

Loading...
Watakiwa kutoa taarifa za tukio lenye shaka - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Watakiwa kutoa taarifa za tukio lenye shaka, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Watakiwa kutoa taarifa za tukio lenye shaka
link : Watakiwa kutoa taarifa za tukio lenye shaka

soma pia


Watakiwa kutoa taarifa za tukio lenye shaka


Mwandishi Wetu

Respicius Timanywa
MKURUGENZI wa shirika lisilo la serikali la Kupunguza Umasikini na Kutunza Mazingira (APEC), Respicius Timanywa, ameomba wananchi kutoa taarifa za mtu au tukio wanalotilia shaka ili kukomesha uhalifu nchini.

Timanywa alitoa mwito huo juzi, kutokana na tukio la uhalifu lililosababisha mauaji ya askari wanane Kibiti mkoani Pwani, wakati akizungumza na madereva wa bodaboda Dar es Salaam kwa kuwahamasisha kulaani mauaji ya polisi.

Mkurugenzi huyo aliwataka wajenge utamaduni wa kujikinga na majanga kwa kuhakikisha wanatoa taarifa kwa wakati, ambapo aliwaeleza kuwa kwa kazi wanayoifanya ni wepesi sana kupata taarifa kirahisi kutokana na mizunguko yao.

Alisema tukio la mauaji ya polisi wanane lililotokea Aprili 13, Mkengeni kata ya Njawa wilayani Kibiti, Pwani lilifanywa na wahalifu, ambao inasadikika wananchi wanatambua maficho yao kwa sababu matukio kama hayo yamekuwa kwenye maeneo hayo kwa muda mrefu.

Alibainisha kuwa wananchi wanatakiwa kujitambua kwa kutoa taarifa za uhalifu mapema, kwa sababu kama zingetolewa mapema na kwa wakati, askari hao wasingepoteza maisha.

"Mafunzo ya kuwajengea uelewa wananchi juu ya umuhimu wa polisi na vituo vya Polisi yatolewe kupitia mradi wa mafunzo ya usalama barabarani, ulinzi shirikishi na ujasiriamali kwa waendesha bodaboda unaoendelea kutekelezwa nchini," alisema Timanywa.

Mkurugenzi huyo aliongeza kuwa mafunzo hayo yatawawezesha kutambua kuwa ulinzi na usalama ni wajibu wa kila Mtanzania, hivyo  kila mtu mwenye taarifa, tukio au mtu anayemtilia shaka apeleke taarifa Polisi mara moja.

“Mbali na Polisi pia mtoe taarifa kwa Ofisa Mtendaji wa Kata, uongozi wa kijiji, mtaa au Mwalimu Mkuu wa Shule ya Msingi au Mkuu wa Sekondari, lengo liwe ni kutokomeza mauaji,” alisema.

Pia aliomba waendesha bodaboda 350,000 waliopewa mafunzo ya usalama barabarani na shirika hilo nchini, kuzindua kampeni ya kulaani mauaji ya polisi na kuhamasisha wananchi kuwa ni wajibu wao kuwakinga.


Hivyo makala Watakiwa kutoa taarifa za tukio lenye shaka

yaani makala yote Watakiwa kutoa taarifa za tukio lenye shaka Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Watakiwa kutoa taarifa za tukio lenye shaka mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/04/watakiwa-kutoa-taarifa-za-tukio-lenye.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Watakiwa kutoa taarifa za tukio lenye shaka"

Post a Comment

Loading...