Loading...

Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa.

Loading...
Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa. - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa., tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa.
link : Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa.

soma pia


Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa.

Na Pascal Mayalla 
 Taasisi ya TradeMark East Africa inazijengea uwezo bidhaa za Tanzania ili  kuziingiza kwenye masoko ya kimataifa, kwa kuziwezesha kukidhi viwango vya ubora wa kimataifa.
Kwa hatua hiyo bidhaa hizo zitakuwa na uwezo wa kuhimili ushindani wa kimataifa na kuingia kwenye masoko ya Nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, Bara la Afrika na masoko ya kimataifa yakiwemo masoko ya Ulaya na Marekani, amesema Mkurugenzi wa TradeMark Tawi la Tanzania, Bw. John Ulanga kwenye kongamano ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es salaam Jumamosi.
Bw. Ulanga amesema zoezi la kuhakikisha bidhaa za Tanzania zinafikia viwango vya ubora wa kimataifa, linafanywa kwa kupitia mafunzo ya viwango vya ubora kwa kuzitumia taasisi za TBC, TFDA na GS 1 kwa ajili ya barcode kwa bidhaa za Tanzania, hivyo bidhaa hizo kuweza kuhimili ushindani katika masoko ya kimataifa kwa kukidhi viwango vya ubora wa kimataifa. 
 Bw. Ulanga amesema mafunzo hayo yanaendeshwa kwa awamu mbalimbali, ni sehemu ya utakelezaji wa mradi mkubwa wa Taasisi ya Trademark East Africa ujulikanao kama “Women in Trade” unaolenga kuwajengea uwezo wafanyabiashara wanawake wa Tanzania, kuhimili ushindani wa kibiashara na kukabiliana na vikwazo vya kibiashara kwa wafanyabiasha wanawake Tanzania kuwawezesha kufanya biashara ya kimataifa ikiwemo kuwezesha bidhaa zao kuyafikia masoko ya nchi za Afrika Mashariki na masoko ya kimataifa ambapo Taasisi ya TradeMark imetenga Dola za Marekani zaidi ya Milioni 5,300,000 ambazo ni zaidi ya Shilingi Bilioni 12 za Kitanzania kugharimia mpango huo.
Mwenyekiti wa TWCC, Mama Jaquline Maleko akizungumza.
Mkurugenzi wa TradeMark East Africa, Tawi la Tanzania, John Ulanga akizungumza kwenye hafla fupi  ya kufungua mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kukidhi viwango vya kimataifavya ubora wa bidhaa, kwa Wafanyabiashara wanawake  wa Tanzania yaliyoandaliwa na Chama cha Wafanyabiashara Wanawake Tanzania (TWCC) ili kuwezesha bidhaa za Tanzania, kuyafikia masoko ya Afrika Mashariki nay a kimataifa. Mafunzo hayo, yameendeshwa na SIDO kwa kushirikiana na taasisi za TBS, TFDA na GS 1 na kufadhiliwa na TradeMark East Africa. Kushoto ni Mwenyekiti wa TWCC, Mama Jaquline Maleko 
 Washirika wa mafunzo hayo,

 Washirika wa mafunzo hayo,
Washirika wa mafunzo hayo, 


Hivyo makala Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa.

yaani makala yote Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa. Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa. mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/05/taasisi-ya-trademark-east-africa-tmea.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Taasisi ya TradeMark East Africa (TMEA) yazijengea Uwezo bidhaa za Tanzania kuingia masoko ya kimataifa."

Post a Comment

Loading...