Loading...

Waomba bajeti ya afya iongezwe

Loading...
Waomba bajeti ya afya iongezwe - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Waomba bajeti ya afya iongezwe, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Waomba bajeti ya afya iongezwe
link : Waomba bajeti ya afya iongezwe

soma pia


Waomba bajeti ya afya iongezwe


Dotto Mwaibale

WANANCHI wameomba bajeti ya mwaka ujao wa fedha ya Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto iongezwe kwa kuzingatia ukubwa wa wizara hiyo.

Wakizungumza Dar es Salaam jana kwenye semina ya siku moja iliyoandaliwa na Mtandao wa Kijinsia Tanzania (TGNP) ya kupitia bajeti hiyo ili kuona vipaumbele vyake, waliomba iongezwe ili kukabiliana na changamoto za wizara hiyo ambayo imelemewa kutokana na ukubwa wake.

Kwa mwaka wa fedha wa 2016/17 Wizara hiyo ilitengewa bajeti ya Sh bilioni 845 ikilinganishwa na mwaka wa fedha wa 2017/18 ambapo jumla kuu ya fedha zote zinazoombwa kwa Wizara hiyo ni Sh. 1,115,608,772,090.

Akizungumza kwenye semina hiyo, Neofita Kunambi alisema katika Wizara hiyo kuna changamoto kubwa na bila kuongezwa fedha hazitakwisha.

"Bila ya kuongeza bajeti katika Wizara hii, wajawazito wataendelea kujinunulia vifaa vya kujifungulia, tunaomba jambo liangaliwe kwa karibu," alisema Kunambi.

Anna Sangai alisema huduma za afya zinapaswa kuboreshwa kuanzia upatikanaji wa dawa na vifaa tiba na bila kuongezwa bajeti katika Wizara hiyo itakuwa ndoto.

Mkazi wa Mbezi Beach, Sadick Juma alisema upatikanaji wa dawa, vifaa tiba, miundombinu na ukatili wa kijinsia ni changamoto kubwa katika Wizara hiyo.

Alisema licha ya kuwepo duka la Bohari Kuu ya Dawa (MSD) katika Hospitali ya Rufaa ya Taifa ya Muhimbili (MNH), upatikanaji wa dawa umekuwa mgumu, hivyo kuifanya Muhimbili kuwa na majengo mazuri bila   dawa.

"Ukitaka kuona changamoto hata ukiwa mwanachama wa Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya (NHIF) ugua au uwe na mgonjwa ambaye ni mwanachama uende katika hospitali hiyo, kwanza kupokewa tu pale Mapokezi ni balaa na ukifika muda wa kutakiwa kupata dawa utaambulia panado na kuambiwa dawa hazipo," alisema Juma.

Juma aliongeza kuwa huduma ya bure kwa watu wenye misamaha hiyo ni ndoto kwani wagonjwa hao hawasikilizwi kabisa jambo ambalo ni hatari.

Alisema Serikali imekuwa ikitamba kuboresha huduma za afya, lakini hali halisi haiko hivyo, akitolea mfano kwa nchi nzima maduka ya dawa ya MSD kuwa manane tu hivyo upatikanaji wa dawa na vifaa tiba kutokidhi mahitaji.

Janeth Mawinza alitaka bajeti hiyo iangalie zaidi jinsi ya kutibu magonjwa kama homa ya ini ambayo matibabu yake nchini hayapatikani mpaka dawa itoke India.

Moses Benard alisema ikiwa mjamzito aliye mjini anatakiwa kujinunulia vifaa vya kujifungulia hali ikoje kwa wa kijijini mwenye changamoto ya kukosa fedha na kukimbiwa na mwenzake, hivyo kuomba Waziri wa Wizara hiyo kutoa tamko rasmi la kutaka wajawazito kutonunua vifaa hivyo wanapokwenda kujifungua.


Hivyo makala Waomba bajeti ya afya iongezwe

yaani makala yote Waomba bajeti ya afya iongezwe Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Waomba bajeti ya afya iongezwe mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/05/waomba-bajeti-ya-afya-iongezwe.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Waomba bajeti ya afya iongezwe"

Post a Comment

Loading...