Loading...
title : Tunaungana na Ulimwengu Kuokoa Bahari- Tizeba
link : Tunaungana na Ulimwengu Kuokoa Bahari- Tizeba
Tunaungana na Ulimwengu Kuokoa Bahari- Tizeba
Na Boss Brown
Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Chares Tizeba ataongoza ujumbe kutoka Tanzania kushiriki katika Kongamano la Bahari Duniani linalotarajiwa kuanza Jumatatu tarehe 5 hadi 9 katika Makao Makuu ya Umoja wa Mataifa New York nchini Marekani.
“Changamoto inayoikabili bahari ni kubwa kutokana na uchafuzi utokanao na taka sugu ambazo zinahatarisha uhai wa Bahari yetu, tunaunagana katika kushilikiana na wadau mbalimbali katika juhudi za kuiokoa bahari kwa pamoja.” Alisisitiza Tizeba.
Akifafanua amesema kama nchi wanachama tanaadhimia kutekeleza kipengele cha 14 cha Malengo ya Maendeleo Endelevu 17 ya agenda ya 2030 ya Umoja wa Mataifa Kinacholenga matumizi bora ya rasilimali za baharini.
Kongamano hili ni la muhimu katika kuokoa bahari na litakutanisha Serikali, Umoja wa Mataifa, Mashirika yasiyo ya Kiserikali, Mashirika yanayoshughulikia mazingira, Taasisi za elimu na wanasayansi ya Jamii, Asasi za Kirai, watu binafsi, makampuni na viwanda.
Sehemu ya fukwe wa Bahari ya Hindi maeneo ya Jiji la Dar es Salaam ikiwa imeathiriwa na uchafu .
Hivyo makala Tunaungana na Ulimwengu Kuokoa Bahari- Tizeba
yaani makala yote Tunaungana na Ulimwengu Kuokoa Bahari- Tizeba Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Tunaungana na Ulimwengu Kuokoa Bahari- Tizeba mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/06/tunaungana-na-ulimwengu-kuokoa-bahari.html
0 Response to "Tunaungana na Ulimwengu Kuokoa Bahari- Tizeba"
Post a Comment