Loading...

WAHANDISI WAZAWA KUHUSISHWA UJENZI BANDARI YA MTWARA

Loading...
WAHANDISI WAZAWA KUHUSISHWA UJENZI BANDARI YA MTWARA - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa WAHANDISI WAZAWA KUHUSISHWA UJENZI BANDARI YA MTWARA, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : WAHANDISI WAZAWA KUHUSISHWA UJENZI BANDARI YA MTWARA
link : WAHANDISI WAZAWA KUHUSISHWA UJENZI BANDARI YA MTWARA

soma pia


WAHANDISI WAZAWA KUHUSISHWA UJENZI BANDARI YA MTWARA

Mwambawahabari


Waziri wa Ujenzi Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa ameuagiza

Uongozi wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA) kupeleka wahandisi wa

kutosha katika ujenzi wa Gati ya Mtwara ili kupata uzoefu katika kazi za ujenzi.




Akizungumza mara baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa Bandari hiyo Waziri

Prof. Mbarawa amesema ushiriki wa wahandisi hao utasaidia kuwajengea uzoefu

mkubwa na hivyo kuokoa fedha nyingi ambazo zitatumika kwa kuwatumia wahandisi wa

kigeni.


“Mradi huu unagharimu fedha nyingi hivyo ni muhimu wahandisi wa TPA wakaja

kujifunza kwa vitendo ili mradi utakapokamilika wahandisi wetu watumike kufanya

ukarabati na matengenezo badala ya kusubiri kuwaleta tena wahandisi kutoka nje”,

amesema Waziri Prof. Mbarawa.


Amesisitiza uongozi wa TPA kutafuta wahandisi waliomaliza vyuo nchini ili waweze

kujifunza kwa vitendo kupitia mradi huo kama sehemu ya mafunzo kwa vitendo ili kupata

uzoefu.


Kwa upande wake, Meneja wa bandari ya Mtwara, Eng. Juma Kijavara, amemhakikishia

Waziri Prof. Mbarawa kuwa tayari utekelezaji wa agizo la kutafuta wahandisi hao

umeshaanza na hatua inayofata ni kuwasili kwa wahandisi hao eneo la madi.


Upanuzi wa bandari ya Mtwara utahusisha awamu nne na awamu ya kwanza ambayo

itagharimu kiasi cha Tsh. bilioni 137 na inatarajiwa kukamilika ndani ya miezi 22,

kukamilika kwa gati hiyo kutaiwezesha bandari hiyo kuhudumia meli ya ukubwa wa mita

300 na kukuza uchumi wa mkoa huo kupitia usafirishaji wa gesi, saruji, korosho pamoja

na makaa mawe.


Meneja wa Bandari ya Mtwara, Eng. Juma Kijavara (kulia), akimuonyesha Waziri wa

Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa, eneo ambalo ujenzi wa

gati ya pili ya bandari hiyo utakapoanza kujengwa wakati Waziri huyo alipokagua vifaa

vya Mkandarasi vilivyowasili katika eneo la mradi hivi karibuni.


Baadhi ya Vifaa ambavyo vitatumika katika ujenzi wa gati ya pili ya bandari ya Mtwara

vikiwa vimeshawekwa site tayari kwa kuanza ujenzi. Ujenzi huo unakadiriwa kukamilika

ndani y amiezi 22.

Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Profesa Makame Mbarawa (mwenye suti

ya Blue), akiangalia vifaa vitakavyotumiwa na Kampuni ya M/S China Railways

Construction Engineering Group (CRCEG) na M/S China Railways Major Bridge

Engineering Group Co. ltd (CRMBEG) katika ujenzi wa gati ya pili ya bandari ya Mtwara,

mkoani humo hivi karibuni.


Hivyo makala WAHANDISI WAZAWA KUHUSISHWA UJENZI BANDARI YA MTWARA

yaani makala yote WAHANDISI WAZAWA KUHUSISHWA UJENZI BANDARI YA MTWARA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala WAHANDISI WAZAWA KUHUSISHWA UJENZI BANDARI YA MTWARA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/06/wahandisi-wazawa-kuhusishwa-ujenzi_30.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "WAHANDISI WAZAWA KUHUSISHWA UJENZI BANDARI YA MTWARA"

Post a Comment

Loading...