Loading...

AGPAHI YAENDESHA KAMPENI YA UPIMAJI MAAMBUKIZI YA VVU MSALALA NA MANISPAA YA SHINYANGA

Loading...
AGPAHI YAENDESHA KAMPENI YA UPIMAJI MAAMBUKIZI YA VVU MSALALA NA MANISPAA YA SHINYANGA - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa AGPAHI YAENDESHA KAMPENI YA UPIMAJI MAAMBUKIZI YA VVU MSALALA NA MANISPAA YA SHINYANGA, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : AGPAHI YAENDESHA KAMPENI YA UPIMAJI MAAMBUKIZI YA VVU MSALALA NA MANISPAA YA SHINYANGA
link : AGPAHI YAENDESHA KAMPENI YA UPIMAJI MAAMBUKIZI YA VVU MSALALA NA MANISPAA YA SHINYANGA

soma pia


AGPAHI YAENDESHA KAMPENI YA UPIMAJI MAAMBUKIZI YA VVU MSALALA NA MANISPAA YA SHINYANGA


Shirika la Ariel Glaser Pediatric Aids Healthcare Initiative (AGPAHI) linalojihusisha na mapambano dhidi ya Virusi vya Ukimwi (VVU) na Ukimwi nchini Tanzania limeendesha Kampeni ya Upimaji wa Maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi kwa watoto na vijana katika halmashauri ya Msalala na Manispaa ya Shinyanga katika mkoa wa Shinyanga. 

Zoezi la kupima watoto na vijana limefanyika Juni 30,2017 na Julai 1,2017 katika zanahati ya Buluma iliyopo katika kijiji cha Buuma kata ya Jana katika halmashauri ya Msalala na zanahati ya kijiji cha Galamba katika kata ya Kolandoto katika manispaa ya Shinyanga.

Zaidi ya watoto na vijana 760 walipata fursa ya kupima afya zao.

Akizungumza wakati wa zoezi hilo la upimaji,Afisa Mradi, Huduma Unganishi kwa Jamii AGPAHI mkoa wa Shinyanga, Charles Simon, alisema kampeni ya Upimaji VVU kwa vijana na watoto yenye kauli mbiu ya “Ijue Afya ya Mwanao” inalenga kuwafikia vijana na watoto wengi zaidi ili kujua afya zao.

“Hili ni zoezi endelevu,AGPAHI kwa kushirikiana na serikali tumekuwa tukipima afya za watoto na vijana na pale inapobainika wamepata maambukizi ya VVU huwa tunawaanzishia huduma ya tiba na matunzo”,alieleza Simon.

Ijumaa Juni 30,2017: Hapa ni katika Zahanati ya Buluma iliyopo katika kijiji cha Buluma kata ya Jana halmashauri ya wilaya ya Msalala mkoa wa Shinyanga .

Afisa Mradi, Huduma Unganishi kwa Jamii AGPAHI mkoa wa Shinyanga, Charles Simon akiwaeleza wazazi na walezi walioleta watoto na vijana katika zahanati ya Buluma kuhusu lengo la Kampeni ya Upimaji wa Maambukizi ya Virusi Vya Ukimwi kwa Watoto na Vijana.

Wazazi,vijana na watoto wakimsikiliza Afisa Mradi, Huduma Unganishi kwa Jamii AGPAHI mkoa wa Shinyanga, Charles Simonwakati akitolea ufafanuzi juu ya kampeni ya Upimaji VVU.

Mratibu wa Wahudumu wa afya ngazi ya Jamii na Upimaji VVU wilaya ya Kahama, Peter Shimba akizungumza kabla ya zoezi la upimaji VVU halijaanza ambapo alilishukuru shirika la AGPAHI katika harakati zake za mapambano dhidi ya VVU na Ukimwi na kwamba serikali itaendelea kushirikiana nalo katika mapambano hayo.



Hivyo makala AGPAHI YAENDESHA KAMPENI YA UPIMAJI MAAMBUKIZI YA VVU MSALALA NA MANISPAA YA SHINYANGA

yaani makala yote AGPAHI YAENDESHA KAMPENI YA UPIMAJI MAAMBUKIZI YA VVU MSALALA NA MANISPAA YA SHINYANGA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala AGPAHI YAENDESHA KAMPENI YA UPIMAJI MAAMBUKIZI YA VVU MSALALA NA MANISPAA YA SHINYANGA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/07/agpahi-yaendesha-kampeni-ya-upimaji.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "AGPAHI YAENDESHA KAMPENI YA UPIMAJI MAAMBUKIZI YA VVU MSALALA NA MANISPAA YA SHINYANGA"

Post a Comment

Loading...