Loading...

Wajasiriamali washiriki miradi ya kujiongeza

Loading...
Wajasiriamali washiriki miradi ya kujiongeza - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Wajasiriamali washiriki miradi ya kujiongeza, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Wajasiriamali washiriki miradi ya kujiongeza
link : Wajasiriamali washiriki miradi ya kujiongeza

soma pia


Wajasiriamali washiriki miradi ya kujiongeza


Mwinyimvua Nzukwi, Zanzibar

Hawra Shamte
WANACHAMA 764 wa vikundi vya ujasiriamali vya wilaya nane za Unguja na Pemba, wameshiriki miradi ya kujiongeza kipato.

Akiwasilisha jana taarifa ya utekelezaji wa Mradi wa Uwezeshaji Wanawake Kiuchumi (WEZA II) awamu ya pili, Meneja Ushawishi na Utetezi wa Chama cha Wanahabari Wanawake Tanzania (TAMWA), Hawra Shamte, alisema hatua hiyo imeamsha ari ya kujiendeleza katika shughuli mbalimbali.

Alisema katika utekelezaji wa mradi huo, wanawake 7,000 kutoka wilaya hizo walipewa mafunzo ya kibiashara, usimamizi wa miradi na kupatiwa nyenzo za uzalishaji, jambo lililowawezesha kupata faida ikilinganishwa na awali katika awamu za kwanza na pili za mradi.

Alisema pamoja na hatua hizo, pia chama hicho kimewezesha wajasiriamali hao kuunda kamati za ngazi ya wilaya, ili kukuza na kufuatilia mwenendo wa biashara zao, kusaka masoko ya bidhaa zao na kujengeana uwezo.

“Kwa lengo la kuwajengea uwezo na kupanua wigo wa biashara zao, TAMWA Zanzibar iliwapeleka wajasiriamali wanne kutoka kamati za biashara za wilaya kwenye maenesho ya kimataifa ya biashara (Sabasaba) yaliyomalizika Dar es Salaam hivi karibuni,” alisema Hawra.

Aidha, alieleza kuwa pamoja na jitihada zinazofanywa na taasisi yake bado baadhi ya wazalishaji wamezoea kuzalisha kizamani kwa kutumia nyenzo duni jambo ambalo linawafanya kushindwa kuhimili ushindani sokoni.

“Miongoni mwa wajasiriamali wanaozalisha bidhaa za matumizi ya nyumbani, vyakula, mapambo, walikuwa wanashindwa kulifikia soko au kuhimili ushindani kutokana na ubora wa bidhaa zao.

“Hivyo ipo haja Serikali kuziona juhudi za wajasiriamali hawa na kuwawezesha kupata vifaa bora vya uzalishaji baada ya sisi kuwapa utaalamu,” alisema Meneja huyo na kuongeza kuwa baadhi ya bidhaa hizo zina ithibati ya ubora.

Akitoa maelezo ya utangulizi kuhusu mradi huo, Ofisa Mradi wa TAMWA Zanzibar, Asha Abdi Makame alisema umelenga kuwajengea uwezo wajasiriamali hao, ili kuendesha na kusimamia miradi yao na kuongeza thamani ya bidhaa zao.

Wajasiriamali hao walieleza kuwa mafunzo na uwezeshaji waliopata umewawezesha kuongeza thamani ya bidhaa zao na kufikia masoko ya nje ya Zanzibar, jambo linaloiwezesha miradi yao kukua na kupata faida kutokana na uzalishaji.


Hivyo makala Wajasiriamali washiriki miradi ya kujiongeza

yaani makala yote Wajasiriamali washiriki miradi ya kujiongeza Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Wajasiriamali washiriki miradi ya kujiongeza mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/07/wajasiriamali-washiriki-miradi-ya.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Wajasiriamali washiriki miradi ya kujiongeza"

Post a Comment

Loading...