Loading...

WAZIRI MKUU ARIDHISHWA NA UJENZI WA GATI YA LINDI

Loading...
WAZIRI MKUU ARIDHISHWA NA UJENZI WA GATI YA LINDI - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa WAZIRI MKUU ARIDHISHWA NA UJENZI WA GATI YA LINDI, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : WAZIRI MKUU ARIDHISHWA NA UJENZI WA GATI YA LINDI
link : WAZIRI MKUU ARIDHISHWA NA UJENZI WA GATI YA LINDI

soma pia


WAZIRI MKUU ARIDHISHWA NA UJENZI WA GATI YA LINDI

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa ametembelea na kufanya ukaguzi katika eneo la mradi wa ujenzi wa gati kwenye Manispaa ya Lindi na kusema kwamba ameridhishwa na utekelezaji wake.

Pia amewaagiza viongozi wa Wakala wa Ufundi na Umeme (TEMESA) mkoa wa Lindi kujenga eneo la kupumzikia abiria kwenye maegesho ya kivuko katika maeneo ya Lindi na Kitunda ili wananchi wa maeneo ya Lindi na Kitunda waanze kupata huduma ya kivuko.

Waziri Mkuu alitembelea mradi huo jana (Ijumaa, Julai 14, 2017) wakati alipotembelea eneo hilo kwa lengo la kukagua maendeleo ya ujenzi wa gati hilo, akiwa katika ziara yake ya kikazi mkoani Lindi.

Alisisitiza kuwa Serikali ya awamu ya tano imedhamiria kuondoa kero ya usafiri kwa wakazi wa maeneo hayo, hivyo ujenzi wa gati hilo uende kwa kasi huku ukizingatia matakwa ya kiufundi na ubora wa hali ya juu.

“Jengeni sehemu ya kupumzikia abiria katika pande zote mbili, upande wa Lindi na wa Kitunda. Mbali na abiria kupata eneo la kupumzikia pia itarahisisha hata ukataji wa tiketi jambo litakawarahisishia ukusanyaji wa mapato.”

Pia Waziri Mkuu aliwaomba wananchi waendelee kuiamini na kushirikiana na Serikali katika shughuli mbalimbali za maendeleo na kwamba ahadi zote zilizoahidiwa katika Ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) zitatekelezwa.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu alimuagiza Mkurugenzi wa Manispaa ya Lindi kuyafanyia maboresho maeneo ya pwani na kuwa ya kisasa kwa kuondoa majengo yote chakavu ili wananchi waweze kuyatumia kwa ajili ya kupumzikia.

Alisema ni vema kwa manispaa hiyo kuainisha majengo yote ya zamani yaliyoko katika upande wa pwani yanayotakiwa kuhifadhiwa kwa ajili ya makumbusho ili yaweze kukarabatiwa na yaliyosalia yaondolewe.

Pia Waziri Mkuu alitembelea chuo cha Chuo cha Ufundi Stadi (VETA) mkoa wa Lindi na kusema kwamba ameridhishwa na utoaji wa elimu chuoni hapo na kuwaagiza viongozi waanzishe mafunzo ya mafuta na gesi ili vijana waweze kupata ujuzi na kuajiriwa kwenye sekta hiyo


Hivyo makala WAZIRI MKUU ARIDHISHWA NA UJENZI WA GATI YA LINDI

yaani makala yote WAZIRI MKUU ARIDHISHWA NA UJENZI WA GATI YA LINDI Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala WAZIRI MKUU ARIDHISHWA NA UJENZI WA GATI YA LINDI mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/07/waziri-mkuu-aridhishwa-na-ujenzi-wa_15.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "WAZIRI MKUU ARIDHISHWA NA UJENZI WA GATI YA LINDI"

Post a Comment

Loading...