Loading...
title : Makamu wa Rais mama Samia awasili Kilimanjaro
link : Makamu wa Rais mama Samia awasili Kilimanjaro
Makamu wa Rais mama Samia awasili Kilimanjaro
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan amewasili mkoani Kilimanjaro na kupokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira pamoja na Viongozi wengine wa Chama na Serikali.
Makamu wa Rais anatazamiwa kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani ambayo Kitaifa yanafanyika mkoani Kilimanjaro kesho Oktoba 16, 2017.
Kauli mbiu ya mwaka huu ni " Zuia Ajali-Tii Sheria Okoa Maisha"
Ufunguzi huo utafanyika katika Uwanja wa Mashujaa uliopo katika Manispaa ya mji wa Moshi.
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akipokelewa na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa KIA ambapo anatazamiwa kuwa mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani. (Picha na Ofisi ya Makamu wa Rais)
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Mhe. Anna Mghwira mara baada ya kuwasili kwenye uwanja wa ndege wa KIA ambapo anatazamiwa kuwa mgeni rasmi katika Maadhimisho ya Wiki ya Nenda kwa Usalama Barabarani.
Hivyo makala Makamu wa Rais mama Samia awasili Kilimanjaro
yaani makala yote Makamu wa Rais mama Samia awasili Kilimanjaro Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala Makamu wa Rais mama Samia awasili Kilimanjaro mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/10/makamu-wa-rais-mama-samia-awasili.html
0 Response to "Makamu wa Rais mama Samia awasili Kilimanjaro"
Post a Comment