Loading...

NAIBU WAZIRI NISHATI AFANYA ZIARA KATIKA KITUO CHA KUPOZA NA KUSAMBAZA UMEME KILICHOPO ZUZU DODOMA

Loading...
NAIBU WAZIRI NISHATI AFANYA ZIARA KATIKA KITUO CHA KUPOZA NA KUSAMBAZA UMEME KILICHOPO ZUZU DODOMA - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa NAIBU WAZIRI NISHATI AFANYA ZIARA KATIKA KITUO CHA KUPOZA NA KUSAMBAZA UMEME KILICHOPO ZUZU DODOMA, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : NAIBU WAZIRI NISHATI AFANYA ZIARA KATIKA KITUO CHA KUPOZA NA KUSAMBAZA UMEME KILICHOPO ZUZU DODOMA
link : NAIBU WAZIRI NISHATI AFANYA ZIARA KATIKA KITUO CHA KUPOZA NA KUSAMBAZA UMEME KILICHOPO ZUZU DODOMA

soma pia


NAIBU WAZIRI NISHATI AFANYA ZIARA KATIKA KITUO CHA KUPOZA NA KUSAMBAZA UMEME KILICHOPO ZUZU DODOMA

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (wa pili kutoka kushoto), akisikiliza maelezo kutoka kwa Kaimu Mkuu wa Kituo cha kupoza na kusambaza umeme kilichopo Zuzu mjini Dodoma, Bosco Mgina (kulia) kuhusu utendaji kazi wa Kituo hicho. Wengine pichani (kutoka kushoto) ni Msaidizi wa Naibu Waziri, Ngereja Mgejwa, Meneja wa TANESCO Mkoa wa Dodoma, Zakayo Temu na Mwendeshaji wa Mitambo katika Kituo hicho, Benedict Stephano.

Na Veronica Simba - Dodoma

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu, amefanya ziara katika Kituo cha kupoza na kusambaza umeme kilichopo eneo la Zuzu mjini Dodoma, leo Oktoba 28, 2017.

Akiwa amefuatana na Meneja wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) Mkoa wa Dodoma, Zakayo Temu, Naibu Waziri Mgalu, ametembelea Kituo hicho ili kujionea utendaji kazi wake.

Akitoa malelezo kwa Naibu Waziri, Kaimu Mkuu wa Kituo hicho, Bosco Mgina amesema kuwa, Kituo hupokea msongo wa umeme wa kilivolti 220 katika njia tatu ambazo ni Mtera, Iringa One na Iringa Two. Aidha, ameongeza kuwa, Kituo kina transfoma mbili za kupoza umeme ambapo kila moja ina uwezo wa kutoa megawati 24 za umeme hivyo kufanya jumla yake kuwa megawati 48.

Akizungumzia hali ya upatikanaji wa umeme kwa Mkoa wa Dodoma, Meneja Temu ameeleza kuwa kwa sasa huduma ya nishati hiyo muhimu imerejea katika maeneo yote baada ya jitihada za Shirika hilo katika kutatua matatizo yaliyojitokeza hivi karibuni.

Akihitimisha ziara yake katika Kituo hicho, Naibu Waziri Mgalu amewasisitiza viongozi wa TANESCO kuhakikisha huduma ya umeme wa uhakika inaendelea kutolewa kwa wateja katika maeneo yote.
Kaimu Mkuu wa Kituo cha kupoza na kusambaza umeme kilichopo Zuzu mjini Dodoma, Bosco Mgina (kushoto), akimwonesha Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (kulia), namna umeme unavyopokelewa kituoni hapo na kusambazwa kwa wateja.
Kaimu Mkuu wa Kituo cha kupoza na kusambaza umeme kilichopo Zuzu mjini Dodoma, Bosco Mgina (kushoto), akifafanua jambo kwa Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu (katikati), wakati Naibu Waziri alipotembelea Kituo hicho kujionea utendaji kazi wake. Kulia ni Meneja wa TANESCO Mkoa wa Dodoma, Zakayo Temu.



Hivyo makala NAIBU WAZIRI NISHATI AFANYA ZIARA KATIKA KITUO CHA KUPOZA NA KUSAMBAZA UMEME KILICHOPO ZUZU DODOMA

yaani makala yote NAIBU WAZIRI NISHATI AFANYA ZIARA KATIKA KITUO CHA KUPOZA NA KUSAMBAZA UMEME KILICHOPO ZUZU DODOMA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala NAIBU WAZIRI NISHATI AFANYA ZIARA KATIKA KITUO CHA KUPOZA NA KUSAMBAZA UMEME KILICHOPO ZUZU DODOMA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/10/naibu-waziri-nishati-afanya-ziara.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "NAIBU WAZIRI NISHATI AFANYA ZIARA KATIKA KITUO CHA KUPOZA NA KUSAMBAZA UMEME KILICHOPO ZUZU DODOMA"

Post a Comment

Loading...