Loading...

Policy Forum wajenga uhusiano mzuri na Serikali katika kuboresha utawala bora

Loading...
Policy Forum wajenga uhusiano mzuri na Serikali katika kuboresha utawala bora - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa Policy Forum wajenga uhusiano mzuri na Serikali katika kuboresha utawala bora, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : Policy Forum wajenga uhusiano mzuri na Serikali katika kuboresha utawala bora
link : Policy Forum wajenga uhusiano mzuri na Serikali katika kuboresha utawala bora

soma pia


Policy Forum wajenga uhusiano mzuri na Serikali katika kuboresha utawala bora

Na Agness Francis, Blogu ya jamii.

Mtandao wa Policy Forum( PF) ambao umetimiza miaka 9 tangu kuanzishwa kwake mwaka 2008 ambapo ilianza kutumia  dhana ya  ufuatiliaji wa uwajibikaji  jamii ( Social Accountability Monitoring) wameungana na wadau katika mkutano wa kujadiliana mafanikio, changamoto  pamoja na mafunzo kutoka kwa wadau mbalimbali wanaotumi dhana hiyo hapa nchini.

Akizungumza hayo leo Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere Kaimu mwenyekiti  Mtandao wa Policy Forum  ( PF), Herbon Mwakagenda amesema kuwa lengo hasa la mkutano huo ni  kuboresha mbinu zinazotumika na wadau  pamoja na kuangalia mafunzo ambayo yanaweza kutumika kwa ujumla ikiwemo pia kutoa pongezi kwa wananchi  kwa kuwa na muamko mkubwa wa kufatilia  haki zao katika mashirika mbalimbali ya Umma. 

Nae pia  Mratibu wa mtandao wa Policy Forum  (PF), Semkae Kilonzo amezungumzia lengo kuwa  ni kutaka  kubadiilishana uzoefu na taasisi mbalimbali ili kuweza kuboresha zaidi   uchechemuzi  wa kutekeleza miradi  yao hapa nchini.

Vile vile Mwenyekiti  Mwakagenda aliongezea hasa kwa kuzungumzi a changamoto zinazo wakabili wakati wa kufikisha ujumbe kwenye Halmashauri  mbalimbali  kutokana na ubadilishwaji wa viongozi wa halmashauri hizo na kusababisha taarifa kuchelewe kufika kama inavyotakiwa.

Diwani Kiteto Manyara,Paulo Tunyon ametoa pongezi za dhati kwa wadau wa  mtandao wa Policy Forum( PF) kwa kuweza kupeleka mabadiliko  Vijijini kwa kukabiliana na changamoto hizo kutokana na uwelewa mdogo wa wananchi hao..
 Kaimu mwenyekiti  Mtandao wa Policy Forum( PF), Herbon Mwakagenda akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mtandao huo jinsi unavyofanya kazi na wadau wa Taasisi mbalimbali hapa nchini leo Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere .
  Mratibu wa mtandao wa Policy Forum ( PF), Semkae Kilonzo  akizungumza na waandishi wa habari kuhusu namna watakavyoweza kukabiliana na changamoto  ili kufikia malengo ya juu zaidi wanayokusudia leo Jijini Dar Es Salaam katika ukumbi wa kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere 
Wadau wa kutoka sehemu mbalimbali hapa nchini waliojitokeza kuhudhuria mkutano huo leo Jijini Dar es Salaam katika ukumbi wa kimataifa wa Julius Kambarage Nyerere




Hivyo makala Policy Forum wajenga uhusiano mzuri na Serikali katika kuboresha utawala bora

yaani makala yote Policy Forum wajenga uhusiano mzuri na Serikali katika kuboresha utawala bora Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala Policy Forum wajenga uhusiano mzuri na Serikali katika kuboresha utawala bora mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/11/policy-forum-wajenga-uhusiano-mzuri-na.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "Policy Forum wajenga uhusiano mzuri na Serikali katika kuboresha utawala bora"

Post a Comment

Loading...