Loading...
title : UVCCM YATAJA MAJINA YA WATAKAOHAKIKI MALI ZA JUMUIYA YAO
link : UVCCM YATAJA MAJINA YA WATAKAOHAKIKI MALI ZA JUMUIYA YAO
UVCCM YATAJA MAJINA YA WATAKAOHAKIKI MALI ZA JUMUIYA YAO
Na Said Mwishehe, Blogu ya Jamii
UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi(UVCCM) imetaja majina sita kati ya wanane ya wajumbe walioteuliwa katika Kamati ya kuchunguza na kufuatilia mali za chama.
Hatua hiyo imekuja kutokana na maagizo ya Mwenyekiti wa Umoja huo Kheir James kutaka kuhakikiwa kwa mali zote za umoja huo.
Akizungumza leo katika Makao Makuu ya umoja huo jijini Dar es Salaam, Katibu Mkuu wa umoja huo Shaka Hamdu Shaka ametaja majina ya wajumbe wa kamati hiyo ambayo itaongozwa na Mwenyekiti Maria Chaurembo.
Wengine ni Peter Kasera, Zelote Saitoti, Rose Manumbu, Sofia Kizigo na Elly Ngowi.
"Jukumu la kamati hiyo ni kufuatilia mali zote za umoja wetu, namna ambavyo zinatumika na mlolongo wa matumizi yake.
" Itaanza kazi haraka na wajumbe wengine wawili wa kamati hii wataungana na wenzao kufanikisha majukumu waliyopewa. Itakapomaliza kazi tutakuja kwenu kuelezea ambacho tumekibaini na nini cha kufanya,"amesema Shaka.
Amesema Mwenyekiti wao baada ya kuchaguliwa kwenye nafasi hiyo moja ya majukumu ambayo ameamua kuanza nayo ni kufuatilia mali za chama na jukumu langu ni kuhakisha maagizo ya mwenyekiti wetu yanafanyiwa kazi tena kwa uhakika,"amesema Shaka.
Hivyo makala UVCCM YATAJA MAJINA YA WATAKAOHAKIKI MALI ZA JUMUIYA YAO
yaani makala yote UVCCM YATAJA MAJINA YA WATAKAOHAKIKI MALI ZA JUMUIYA YAO Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala UVCCM YATAJA MAJINA YA WATAKAOHAKIKI MALI ZA JUMUIYA YAO mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/12/uvccm-yataja-majina-ya-watakaohakiki.html
0 Response to "UVCCM YATAJA MAJINA YA WATAKAOHAKIKI MALI ZA JUMUIYA YAO"
Post a Comment