Loading...

VIONGOZI WA UMMA WATAKIWA KUKABIDHI ORODHA YA MALI ZAO KABLA YA DESEMBA 31

Loading...
VIONGOZI WA UMMA WATAKIWA KUKABIDHI ORODHA YA MALI ZAO KABLA YA DESEMBA 31 - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa VIONGOZI WA UMMA WATAKIWA KUKABIDHI ORODHA YA MALI ZAO KABLA YA DESEMBA 31, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : VIONGOZI WA UMMA WATAKIWA KUKABIDHI ORODHA YA MALI ZAO KABLA YA DESEMBA 31
link : VIONGOZI WA UMMA WATAKIWA KUKABIDHI ORODHA YA MALI ZAO KABLA YA DESEMBA 31

soma pia


VIONGOZI WA UMMA WATAKIWA KUKABIDHI ORODHA YA MALI ZAO KABLA YA DESEMBA 31

VIONGOZI

wote wa umma nchini wametakiwa kuorodhesha mali zao tena kwa usahihi na
kisha kukabidhi kwa Sekretarieti ya Maadili ya Viongozi wa Umma kabla 
ya Desemba 31 mwaka huu. 

Wamesisitiza kufanya hivyo ni utaratibu
ambao upo kwa mujibu wa sheria ,hivyo lazima watekeleze kwa wakati na 
watakaoshindwa hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

 

 Hayo
yamesemwa Dar es Salaam leo na Kamishna wa Sekretarieti ya Maadili ya 
Viongozi wa Umma, Jaji Mstaafu Harold Nsekela wakati akitangza tarehe ya
mwisho kwa viongozi wa umma kukabidhi tamko la mali zao ambayo ni 
Desemba 31 mwaka huu. 

“Kila kiongozi wa umma ajaze tamko hilo 
kwa kuorodhesha mali zake, mwenza wake na watoto wake walio na umri 
chini ya miaka 18,”amesema. Amefafanua viongozi wanaotakiwa kuorodhesha
mali zao na kisha kukabidhi Sekretarieti ya Maadili ni wale wa 
kuteuliwa na kuchaguliwa. 

“Pia ujazaji wa tamko hilo kisheria 
linawahusisha hata viongozi waliostaafu na wale wanaoelekea 
kustaafu,”amesisitiza. Ameongeza viongozi ambao wanastaafu wakati 
wanaingia waliorodhesha mali zao, hivyo wanapostaafu ni lazima 
waoredheshe ili ifahamike wanatoka wakiwa na mali kiasi gani. 

“Hivyo
ni muhimu kila kiongozi kujaza hilo tamko na tunachokifanya sisi ni 
kukumbusha tu.Fomu za tamko zipo kwenye tovuti ya sekretarieti ya 
maadili. “Huko nyuma tulikuwa tunawatafuta viongozi na kuwapa matamko 
wajaze lakini sasa ni lazima wao kuchukua na kujaza na jukumu letu ni 
kupokea na kisha kuchambua tamko la kila kiongozi,”amesema Jaji mstaafu 
Nsekela. 

Amesema anaamini viongozi wanafahamu wajibu wao,hivyo 
wafanye haraka iwezekanavyo na hasa kwa kuzingatia muda uliobakia ni 
mchache. Alipoulizwa ni viongozi wangapi wamejaza fomu hadi sasa,Jaji 
mstaafu Nsekela amesema hana takwimu sahihi lakini baada ya muda 
ulioapngwa kumaliza watatoa taarifa sahihi huku akieleza yeye tayari 
ameorodhesha mali zake kwenye tamko na kukabidhi tena kwa Rais. 

Kuhusu
viongozi wanaostaafu ambao wamejaza tamko hilo amesema nao bado lakini 
katika eneo hilo kuna changamoto yake kidogo kwani viongozi wanapostaafu
inakuwa ngumu kuwapata lakini nao watambue wanatakiwa kujaza tamko kwa 
mujibu wa sheria. 

Kwa upande wake, Ofisa Sheria Mkuu wa 
Sekretarieti ya Mmaadili Bw. Filotheus Manula ameongeza ujazaji wa 
tamko la mali kwa viongozi wa umma ni takwa la kikatiba na kuna adhabu 
kwa wasiofuata. 

Ametaja adhabu hizo ni kuonywa, kushushwa cheo, kusimamishwa kazi na wakati mwingine kufukuzwa Nazi.

Na Said Mwishehe,Blogu ya Jamii 




Hivyo makala VIONGOZI WA UMMA WATAKIWA KUKABIDHI ORODHA YA MALI ZAO KABLA YA DESEMBA 31

yaani makala yote VIONGOZI WA UMMA WATAKIWA KUKABIDHI ORODHA YA MALI ZAO KABLA YA DESEMBA 31 Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala VIONGOZI WA UMMA WATAKIWA KUKABIDHI ORODHA YA MALI ZAO KABLA YA DESEMBA 31 mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2017/12/viongozi-wa-umma-watakiwa-kukabidhi_27.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "VIONGOZI WA UMMA WATAKIWA KUKABIDHI ORODHA YA MALI ZAO KABLA YA DESEMBA 31"

Post a Comment

Loading...