Loading...

DC SHINYANGA AFANYA MKUTANO KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI BUGAYAMBELELE

Loading...
DC SHINYANGA AFANYA MKUTANO KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI BUGAYAMBELELE - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa DC SHINYANGA AFANYA MKUTANO KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI BUGAYAMBELELE, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : DC SHINYANGA AFANYA MKUTANO KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI BUGAYAMBELELE
link : DC SHINYANGA AFANYA MKUTANO KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI BUGAYAMBELELE

soma pia


DC SHINYANGA AFANYA MKUTANO KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI BUGAYAMBELELE

Mkuu wa wilaya ya Shinyanga amewataka maafisa watendaji wa vijiji na kata kusoma taarifa za mapato na matumizi kwa wananchi pamoja na wenyeviti wa vitongoji,mitaa,vijiji na kata kufanya mikutano kwa ajili ya kutatua kero zinazowakabili wananchi. 

Matiro ametoa agizo hilo leo Jumatatu Februari 26,2018 wakati wa mkutano wa kusikiliza kero za wananchi akiwa ameambatana na maafisa mbalimbali wa halmashauri ya manispaa ya Shinyanga katika kijiji cha Bugayambelele kata ya Kizumbi katika manispaa ya Shinyanga.

Alitoa agizo hilo baada ya wananchi kudai kuwa viongozi waliopo katika kata hiyo hawafanyi mikutano kusikiliza kero za wananchi na badala yake wamekuwa wakisubiri uchaguzi ukikaribia ndiyo wanajitokeza.

Mmoja wa wananchi hao,Paul Kashinje (87) alisema viongozi wa eneo hilo hawawajibiki kwa wananchi matokeo yake wamekuwa wakikabiliwa na changamoto lukuki na kutoa tahadhari kuwa kipindi hiki wanataka vitendo zaidi kuliko maneno kwa viongozi hao na wasipobadilika watawashughulikia.

Kufuatia hoja hiyo na zingine,Matiro aliwaagiza viongozi wa vitongoji,vijiji,mitaa na kata kuhakikisha wafanya mikutano na wananchi ili kujadili namna ya kutatua kero zao huku akiagiza maafisa watendaji kusoma taarifa za mapato na matumizi ili kuondoa migongano isiyokuwa ya lazima.

Katika hatua nyingine Matiro alitumia fursa hiyo kuwahamasisha wananchi kujenga nyumba bora badala ya kuishi kwenye nyumba za udongo ambazo ni rahisi kubomoka inaponyesha hata mvua kidogo tu.

Matiro pia aliwataka wananchi kutunza mazingira kwa kupanda miti na kuitunza na kulima zao la mtama badala ya kulima mahindi ambayo ustawi wake siyo mzuri mkoani Shinyanga.

Wakizungumza mbele ya mkuu wa wilaya,wananchi walizitaja baadhi ya kero zao kuwa ni kukosekana kwa eneo la mazishi “makaburi”,ukosefu wa shule,barabara,zahanati,maji,umeme na migogoro ya viwanja.
Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro (kulia) akimsikiliza kwa makini mwananchi mkazi wa kijiji cha Bugayambelele akielezea jinsi anavyoteseka kupata huduma ya maji. Picha zote na Kadama Malunde - Malunde1 blog.
Mzee Paul Kashinje akieleza kero yake kwa mkuu wa wilaya ya Shinyanga, Josephine Matiro ...Alisema "Viongozi wetu hawafanyi chochote,ujio wako hapa naamini utasaidia...Tumechoka na maneno yao,tunahitaji vitendo,bila vitendo tunawashughulikia".
William Mlori akielezea kero ya viwanja na ardhi.
Wananchi wakimsikiliza Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Josephine Matiro 


Hivyo makala DC SHINYANGA AFANYA MKUTANO KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI BUGAYAMBELELE

yaani makala yote DC SHINYANGA AFANYA MKUTANO KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI BUGAYAMBELELE Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala DC SHINYANGA AFANYA MKUTANO KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI BUGAYAMBELELE mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/02/dc-shinyanga-afanya-mkutano-kusikiliza.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "DC SHINYANGA AFANYA MKUTANO KUSIKILIZA KERO ZA WANANCHI BUGAYAMBELELE"

Post a Comment

Loading...