Loading...
title : KWANDKWA: SERIKALI KUIMARISHA SEKTA YA UJENZI NA UCHUKUZI MKOA WA TANGA
link : KWANDKWA: SERIKALI KUIMARISHA SEKTA YA UJENZI NA UCHUKUZI MKOA WA TANGA
KWANDKWA: SERIKALI KUIMARISHA SEKTA YA UJENZI NA UCHUKUZI MKOA WA TANGA
Na Ismail Ngayonga -MAELEZO
NAIBU Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa amesema Serikali imekusudia kuimarisha sekta ya ujenzi na uchukuzi katika Mkoa wa Tanga ikiwemo Ujenzi wa Daraja kubwa lenye urefu wa Mita 550 katika Wilaya ya Pangani, hatua inayolenga kufungua fursa na kuinua pato la kiuchumi kwa wanachi wa Mkoa huo.
Akizungumza katika mkutano wake na Mkuu wa Mkoa huo, Martin Sheghela jana Jumanne Februari 12, 2018, Naibu Waziri Kwandikwa aliyopo katika ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya barabara Mkoani humo, alisema lengo la Serikali ni kuimarisha miundombinu ya barabara, bandari na uwanja wa ndege katika Mkoa wa Tanga.
Kwandikwa alisema katika bajeti ya mwaka 2017/18 Serikali imekusudia kuanza ujenzi wa barabara ya Tanga-Pangani-Saadani-Bagamoyo yenye urefu urefu wa kilometa 242, ambapo tayari kazi ya usanifu wa barabara hiyo tayari umeaanza, ambapo wakati wowote kutoka sasa Serikali inatarajia kutangaza zabuni ya ujenzi wa barabara hiyo.
“Kwa kipande cha barabara ya Tanga-Pangani ambayo imekuwa kilio cha wananchi wa Pangani kwa kipindi kirefu, tayari tumeanza hatua ya usanifu wa barabara hiyo, ambapo Serikali imetenga kiasi cha Tsh. Bilioni 4.3 kwa ajili ya ujenzi wa barabara hiyo” alisema Kwandikwa.
Meneja wa TANROAD Mkoa wa Tanga, Mhandisi Alfred Ndumbaro akitoa maelezo ya ufafanuzi kwa Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa (wa pili kulia)kuhusu ujenzi wa Daraja kubwa lenye urefu wa kilometa 550 linalotarajia kujengwa na Serikali katika Mto Pangani wakati wa ziara yake Wilayani humo jana Jumanne Februari 13 2018. Kulia ni Mkuu wa Wilaya hiyo, Bi. Zainab Issa.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa akipata maelezo kuhusu ufafanisi wa utendaji kazi wa kivuko cha MV Tanga wakati wa ziara yake ya kukagua miradi ya barabara na vivuko katika Wilaya ya Pangani na Mkoa wa Tanga kwa ujumla katika ziara yake jana Jumanne Februari 13 2018. Kulia ni Meneja wa Wakala wa Ufundi na Umeme Serikalini (TEMESA), Mhandisi Magreth Ginna.
Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Elias Kwandikwa akishuka katika kivuko cha MV Tanga iliyopo Pangani wakati wa Ziara yake ya kukagua miradi mbalimbali ya barabara na vivuko katika Wilaya za Mkoa wa Tanga jana Jumanne Februari 13, 2018. Anaongoza nao Diwani wa Kata ya Pangani Magharibi, John Semhande na Meneja wa TEMESA Mkoa wa Tanga, Mhandisi Magreth Ginna na Mkuu wa Wilaya ya Pangani Zainab Issa. (PICHA NA MAELEZO
Hivyo makala KWANDKWA: SERIKALI KUIMARISHA SEKTA YA UJENZI NA UCHUKUZI MKOA WA TANGA
yaani makala yote KWANDKWA: SERIKALI KUIMARISHA SEKTA YA UJENZI NA UCHUKUZI MKOA WA TANGA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala KWANDKWA: SERIKALI KUIMARISHA SEKTA YA UJENZI NA UCHUKUZI MKOA WA TANGA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/02/kwandkwa-serikali-kuimarisha-sekta-ya.html
0 Response to "KWANDKWA: SERIKALI KUIMARISHA SEKTA YA UJENZI NA UCHUKUZI MKOA WA TANGA"
Post a Comment