Loading...

UWT YAUNGA MKONO KAULI YA RAIS MAGUFULI KUZUIA MAANDAMANO

Loading...
UWT YAUNGA MKONO KAULI YA RAIS MAGUFULI KUZUIA MAANDAMANO - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa UWT YAUNGA MKONO KAULI YA RAIS MAGUFULI KUZUIA MAANDAMANO, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : UWT YAUNGA MKONO KAULI YA RAIS MAGUFULI KUZUIA MAANDAMANO
link : UWT YAUNGA MKONO KAULI YA RAIS MAGUFULI KUZUIA MAANDAMANO

soma pia


UWT YAUNGA MKONO KAULI YA RAIS MAGUFULI KUZUIA MAANDAMANO

*Watangaza vipaumbele vinne watakavyoanza navyo
*Waomba viongozi kutoa kauli za kudumisha mshikamano

Na Said Mwishehe,Globu ya Jamii

KAMATI ya Utekelezaji ya Baraza Kuu la Jumuiya ya Wanawake Tanzania(UWT)kwa kauli moja wamempongeza Rais John Magufuli kwa kauli yake ya kuzuia maandamano nchini na kusisitiza wanawake wa Tanzania hawapo tayari kuandamana.

Pia wamempongeza Rais Magufuli na Rais wa Zanzibar Dk.Ali Mohammed Shein kwa usimamizi mzuri wa Ilani ya Chama Cha Mapinduzi(CCM)kwani wamefanikisha uchumi wa Tanzania kuimarika.Pamoja na hayo Kamati hiyo imetangaza kuanza kazi rasmi za UWT ambapo kati ya vipaumbele ambavyo wamepanga kuvifanya kwa kipindi cha miaka mitano ni 18 lakini wametangaza na vipaumbele vinne.

Hayo yamesemwa Dar es Salaam leo na Mwenyekiti wa UWT Gaudentia Kabaka wakati akitangaza maazimio ya kikao cha Kamati ya Baraza Kuu la jumuiya hiyo.

WAKATAA MAANDAMANO

Akizungumzia kauli ya Rais Magufuli ya kuzuia maandamano nchini,Kabaka amesema wanaukanga mkono kauli hiyo na kusisitiza kuwa wanawake wa Tanzania hawapo tayari kushiriki kwenye kufanya maandamano.

Amesema kuwa jukumu la wanawake wa Tanzania ni kufanya kazi kwa bidii ili kuhakikisha nchi inapiga hatua kimaendeleo na kwamba wanalaani kauli za baadhi ya viongozi na watu wengine ambao wamekuwa wakitoa lugha zinazoashiria uvunjifu wa amani nchini.

"Tunaomba viongizi wa dini na viongozi wa kimila kuhakikisha wanatoa kauli za kujenga na kuhamasisha umoja,amani ,upendo ,heshima na mshikamano." Tunampongeza Rais Magufuli na Rais Shein kwa kuendelea kukemea watu wasiotakia nchi yetu iwe na amani kwa kutaka kufanya maandamano au matamko ya uchochezi,"amesema Kabaka.

Ameongeza kuwa "Watanzania hatuna muda wa maandamano ,tuna muda wa kufanya kazi ili kujiletea maendeleo ya nchi yetu tajiri,"amesema.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya Wanawake Tanzania(UWT)Gaudentia Kabaka(katikati)akizungumza na waandishi wa habari leo jijini Dar es Salaam wakati akielezea maazimio ya Kamati ya Utekelezaji wa Baraza Kuu la jumuiya iliyokutana leo.Picha na said Mwishehe.




Hivyo makala UWT YAUNGA MKONO KAULI YA RAIS MAGUFULI KUZUIA MAANDAMANO

yaani makala yote UWT YAUNGA MKONO KAULI YA RAIS MAGUFULI KUZUIA MAANDAMANO Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala UWT YAUNGA MKONO KAULI YA RAIS MAGUFULI KUZUIA MAANDAMANO mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/03/uwt-yaunga-mkono-kauli-ya-rais-magufuli.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "UWT YAUNGA MKONO KAULI YA RAIS MAGUFULI KUZUIA MAANDAMANO"

Post a Comment

Loading...