Loading...
title : UBONGO LEARNING YAKABILIANA NA UWEZO WA VIJANA WA KITANZANIA KUPATA AJIRA
link : UBONGO LEARNING YAKABILIANA NA UWEZO WA VIJANA WA KITANZANIA KUPATA AJIRA
UBONGO LEARNING YAKABILIANA NA UWEZO WA VIJANA WA KITANZANIA KUPATA AJIRA
Ubongo Learning ambalo ni shirika linaloongoza barani Afrika kwa maudhui ya elimu ya kuburudisha kwa watoto, leo imeandaa mkutano wake wa mwaka ambao ulikuwa na lengo ya kuzungumzia uwezeshwaji kiuchumi, haswa kwa wasichana ambao wanaweza kuathirika zaidi ya wavulana kutokana na mabadiliko katika soko la ajira.
Kwa kipindi cha miezi 6 sasa, Ubongo Learning, shirika lisilo la kibiashara ambalo ndiyo lilibuni katuni za kuelimisha za Ubongo Kids, limekuwa likifanya utafiti juu ya uwezo wa kupata ajira na usimamizi wa fedha miongoni mwa vijana nchini Tanzania.
Kwa kipindi cha miezi 6 sasa, Ubongo Learning, shirika lisilo la kibiashara ambalo ndiyo lilibuni katuni za kuelimisha za Ubongo Kids, limekuwa likifanya utafiti juu ya uwezo wa kupata ajira na usimamizi wa fedha miongoni mwa vijana nchini Tanzania.
Lengo la mradi huu, uliofadhiliwa na Data for Local Impact (DLI), ni kuelimisha vijana, haswa wasichana jinsi ya kutumia maelezo, taarifa na takwimu zinazopatikana ili kufanya maamuzi bora juu ya maisha yao ya mbeleni, na zaidi ya hilo kupitia ujuzi wa masala ya kifedha. Vipindi vya televisheni vya Ubongo vinatazamwa na zaidi ya watu milioni 6.4 kila mwezi, hivyo kuvifanya kuwa vipindi vya watoto vyenye watazamaji wengi kuliko vyote Afrika Mashariki na kuwa sehemu nzuri sana kuwasilisha maswala muhimu kwa vijana.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano huo, Meneja Masoko Ubongo Learning Iman Lipumba alisema licha ya kuwa na Maendeleo makubwa ya kuhakikisha wasichana wanaandikishwa shule za msingi, lakini bado jamii nyingi nchini Tanzania bado zinawapendelea wavulana kielimu (hususan kwenye elimu ya shule za sekondari na vyuo vikuu) zaidi ya wasichana.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano huo, Meneja Masoko Ubongo Learning Iman Lipumba alisema licha ya kuwa na Maendeleo makubwa ya kuhakikisha wasichana wanaandikishwa shule za msingi, lakini bado jamii nyingi nchini Tanzania bado zinawapendelea wavulana kielimu (hususan kwenye elimu ya shule za sekondari na vyuo vikuu) zaidi ya wasichana.
Zaidi ya hilo, utafiti wetu unaonyesha kuwa wavulana wanashawishiwa zaidi kusoma masomo ya sayansi, hesabu na ukandarasi, taaluma ambazo zinahitajika sana katika soko la ajira, na wasichana wanashauriwa kuingia kwenye masomo ya sanaa na hatimaye kufanya kazi za utoa huduma ambazo huenda zikapotea katika miaka michache ijayo.
Mwakilishi wa Catholic Relief Service,Priyanka Jagtap, akiwasilisha mada katika mkutano wa mwaka wa Shirika lilisilo la Kiserikali la Ubongo Learning linalojishughulisha na elimu ya kuburudisha watoto. Mkutano huo ulikuwa na lengo ya kuzungumzia uwezeshwaji kiuchumi, haswa kwa wasichana ambao wanaweza kuathirika zaidi ya wavulana kutokana na mabadiliko katika soko la ajira leo jijini Dar es Salaam
Ofisa Mtendaji Mkuu wa Shirika lilisilo la Kiserikali la Ubongo Learning linalojishughulisha na elimu ya kuburudisha watoto, Nisha Lagon, akiwasilisha mada katika mkutano wake wa mwaka ambao ulikuwa na lengo ya kuzungumzia uwezeshwaji kiuchumi, haswa kwa wasichana ambao wanaweza kuathirika zaidi ya wavulana kutokana na mabadiliko katika soko la ajira leo jijini Dar es Salaam.Kulia ni Mwakilishi wa Catholic Relief Service,Priyanka Jagtap.
Mwakilishi wa BBC Media Action ,Doreen Bangapi,akichangia mada katika katika mkutano wa mwaka wa wadau wa mwaka wa Shirika lilisilo la Kiserikali la Ubongo Learning linalojishughulisha na elimu ya kuburudisha watoto. Mkutano huo ulikuwa na lengo ya kuzungumzia uwezeshwaji kiuchumi, haswa kwa wasichana ambao wanaweza kuathirika zaidi ya wavulana kutokana na mabadiliko katika soko la ajira leo jijini Dar es Salaam.
Hivyo makala UBONGO LEARNING YAKABILIANA NA UWEZO WA VIJANA WA KITANZANIA KUPATA AJIRA
yaani makala yote UBONGO LEARNING YAKABILIANA NA UWEZO WA VIJANA WA KITANZANIA KUPATA AJIRA Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala UBONGO LEARNING YAKABILIANA NA UWEZO WA VIJANA WA KITANZANIA KUPATA AJIRA mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/05/ubongo-learning-yakabiliana-na-uwezo-wa.html
0 Response to "UBONGO LEARNING YAKABILIANA NA UWEZO WA VIJANA WA KITANZANIA KUPATA AJIRA"
Post a Comment