Loading...
title : HIMID MAO MKAMI AAGA RASMI AZAM FC
link : HIMID MAO MKAMI AAGA RASMI AZAM FC
HIMID MAO MKAMI AAGA RASMI AZAM FC
Na Bakari Madjeshi, Globu ya Jamii
Aliyekuwa Nahodha wa Azam FC, Himid Mao Mkami ameiaga rasmi timu hiyo, baada yakupata nafasi kwenda kucheza Soka la kulipwa nchini Misri kwenye Klabu ya Petrojet inayoshiriki Ligi Kuu nchini humo inayofundishwa na Aliyekuwa Kocha wa timu ya taifa ya Misri, Hassan Shehata.
Himid maarufu kwa jina la Ninja aliyekuwa na Azam FC tangu mwaka 2009, katika ukurasa wake wa Instagram ametumia nafasi hiyo kuaga Benchi la Ufundi, Makocha, Viongozi na Wafanyakazi wote wa timu hiyo iliyomaliza nafasi ya pili kwenye Ligi Kuu Soka Tanzania Bara (VPL).
‘Nashukuru kufanya kazi pamoja kila siku kwa ushirikiano na timu ya Azam katika kupanda na kushuka, huzuni na furaha na bado mlikua bega kwa bega na mimi miaka yote, ni huzuni kusema kwa heri lakini haikuwa na jinsi’, ameandika Himid Mao.
Himid amesema alifanya maamuzi kwa kushirikiana na uongozi wa timu hiyo na kumruhusu alipoomba ruhusa yakutafuta changamoto mpya.
Hivyo makala HIMID MAO MKAMI AAGA RASMI AZAM FC
yaani makala yote HIMID MAO MKAMI AAGA RASMI AZAM FC Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala HIMID MAO MKAMI AAGA RASMI AZAM FC mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/06/himid-mao-mkami-aaga-rasmi-azam-fc.html
0 Response to "HIMID MAO MKAMI AAGA RASMI AZAM FC"
Post a Comment