Loading...
title : HESLB yajipanga kuongeza ufanisi
link : HESLB yajipanga kuongeza ufanisi
HESLB yajipanga kuongeza ufanisi
Na Chalila Kibuda, Globu ya Jamii
Mkurugenzi Mtendaji wa HESLB Abdul-Razaq Badru amesema wameyapokea maoni ya wadau na watayafanyia kazi ili kuongeza ufanisi katika utoaji na urejeshaji wa mikopo.
Badru aliyasema hayo wakati akizungumza katika banda la Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), kwenye maonesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa katika viwanja vya Mwalimu Julius Nyerere. Amesema kuwa HESLB inashiriki katika maonesho hayo kwa lengo la kutoa elimu kwa wazazi, wanafunzi pamoja wanufaika wa mikopo.
Amesema kuwa wadau wakifika katika banda la bodi watapata ufafanuzi wa vipengele kwa waombaji mikopo katika bodi hiyo utakaomalizika Julai 15 mwaka huu kwa waombaji hao kupata taarifa sahihi.
Badru amesema kuwa wanufaika wa mikopo pia watapata elimu ya urejeshaji wa mikopo iliyoiva ili kuweza kurejesha katika mfuko kwa ajili wengine kunufaika ikiwa ni pamoja na kujua ankara zao kwa ajili ya kulipa kutokana na kuwepo na changamoto katika malipo.
Badru amesema kuwa wanufaika wa mikopo pia watapata elimu ya urejeshaji wa mikopo iliyoiva ili kuweza kurejesha katika mfuko kwa ajili wengine kunufaika ikiwa ni pamoja na kujua ankara zao kwa ajili ya kulipa kutokana na kuwepo na changamoto katika malipo.
Aidha amesema kuwa baadhi ya waajiri wamekuwa na mwamko wa kukata asilimia 15 ya mshahara huku wengine wakikata bila kupeleka bodi kwa wakati muafaka.Amesema waajiri ambao wamekuwa wakishindwa kufanya malipo kwa wafanyakazi wao wamekuwa wakiwapeleka mahakamani na wakifika huko wanaomba wazungumze nje ya mahakama na matokeo yake wanalipa.
01.Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), Abdul-Razaq Badru akizungumza na Mwandishi wa Michuzi Blog katika banda la bodi hiyo katika maonesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa katika viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB), Abdul-Razaq Badru akiwapa huduma wananchi waliotembelea banda la bodi katika maonesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa katika viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
Mkuu wa Chuo Kikuu cha Aga Khan Prof. Joe Lugalla akipata maelezo katika banda la bodi ya mikopo alipotembelea maonesho ya 42 ya Biashara ya Kimataifa katika viwanja vya Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Hivyo makala HESLB yajipanga kuongeza ufanisi
yaani makala yote HESLB yajipanga kuongeza ufanisi Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala HESLB yajipanga kuongeza ufanisi mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/07/heslb-yajipanga-kuongeza-ufanisi.html
0 Response to "HESLB yajipanga kuongeza ufanisi"
Post a Comment