Loading...

WAZAZI, WALEZI WATAKIWA KUFICHUA WATOTO WENYE ULEMAVU

Loading...
WAZAZI, WALEZI WATAKIWA KUFICHUA WATOTO WENYE ULEMAVU - Hallo rafiki SOMA LATEST, Katika makala kusoma wakati huu na kichwa WAZAZI, WALEZI WATAKIWA KUFICHUA WATOTO WENYE ULEMAVU, tumeandaa vizuri kwa makala hii kusoma na kupakua maelezo humo. pengine kujaza posts makala afya, makala general, makala kisiasa, makala kitamaduni, makala kiuchumi, makala mambo mapya, makala michezo, sisi kuandika anaweza kuelewa. Naam, furaha ya kusoma.

title : WAZAZI, WALEZI WATAKIWA KUFICHUA WATOTO WENYE ULEMAVU
link : WAZAZI, WALEZI WATAKIWA KUFICHUA WATOTO WENYE ULEMAVU

soma pia


WAZAZI, WALEZI WATAKIWA KUFICHUA WATOTO WENYE ULEMAVU

Na Frankius Cleophace, Serengeti

KATA ya Manchira wilayani Serengeti mkoani Mara wameendelea kuwabaini watoto wenye ulemavu wa aina yeyote ili wapelekwe shule kwa lengo la kupata haki zao kama watoto wengine.

Hivyo wazazi na walezi wilayani humo wametakiwa kuendelea kufichua watoto wenye ulemabu ili nao wapate haki ya kupata elimu.

Hayo yamebainishwa na Ofisa Elimu Kata ya Machira  Fidel Sylivanus wakati wa tamasha lililoandaliwa na Shirika la RIGHT TO PLAY kwa lengo ni  kutoa elimu kwa jamii ili kuondokana na mila zenye madhara  ukiwemo ukeketaji kwa mtoto wa kike.Sylivanus amesema katika kata nzima tayari wamezunguka  na kubaini watoto wenye ulemavu wa aina yeyote na kuwataka wazazi na walezi kufichua watoto hao.
 
Pia amewahamiza wazazi na walezi suala la elimu kwa watoto wote bila ubaguzi wa jinsia ni muhimu huku watoto wakitaja changamoto kubwa kuwa ni wazazi kuwapatia kazi nyingi na kushindwa kufanya michezo  na kujisomea.Leah Kimaro kutoka Shirika la RIGHT TO PLAY  amesema  takribani Siku Nne amabazo shirika hilo limefanya matamasha wamefikia wananchi takribani 5000Elfu na kuweza kuwapatia ujumbe uliokusudiwa kupitia michezo mbalimbali.

 Amesema michezo hiyo iliambatana na maombi, Ngonjera, Maigizo, Mpira wa miguu kwa watoto wakike, kukimbiza kuku na kukimbia ndani ya magumia na kwamba lengo ni kukusanya jamii ili kupatiwa elimu hiyo.Aidha wananchi wamekuwa na maoni tofauti kuhusu matamasha hayo ambao yameandaliwa na Shirika la RIGHT TO PLAY kwa siku nne na kutoa elimu ilikusudiwa katika jamii wilayani Serengeti mkoani Mara.

Ambapo wameomba kuwa matamasha hayo yawe endelevu katika maeneo ya vijijini ili kuendelea kutoa elimu Katika wilaya hiyo. 
Wanafunzi wa Shule ya Msingi Miseke na Wananchi wakata ya Manchira Wilayani Serengeti Mkoani Mara wakiwa katika Maandamano na Mabango yenye ujumbe mbalimbali wa kupiga Vita Ukatili kwa watoto kwenye Tamasha la Michezo lililoandaliwa na Shirika la RIGHT TO PLAY lililopo Serengeti Mkoani Mara.
Afisa Elimu kata ya Manchira Fidelis Sylivanus akisalimiana na Timu ya Mpira wa Miguu Miseke Wakubwa FC na Miseke Wadogo FC.
Afisa Elimu kata ya Manchira Fidelis Sylivanus akisalimiana na Timu ya Mpira wa Miguu wa Wasichana baina ya Timu Miseke FC na Bwitenge FC katika Viwanja vya Shule ya Msingi Miseke.
Mgeni rasmi ambaye ni Afisa Elimu Kata ya Manchira Fidels Syilivanusi akikabidhi zawadi mbalimbali kwa Washiriki wa Michezo hiyo.


Hivyo makala WAZAZI, WALEZI WATAKIWA KUFICHUA WATOTO WENYE ULEMAVU

yaani makala yote WAZAZI, WALEZI WATAKIWA KUFICHUA WATOTO WENYE ULEMAVU Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.

Wewe ni sasa kusoma makala WAZAZI, WALEZI WATAKIWA KUFICHUA WATOTO WENYE ULEMAVU mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/07/wazazi-walezi-watakiwa-kufichua-watoto.html

Subscribe to receive free email updates:

Related Posts :

0 Response to "WAZAZI, WALEZI WATAKIWA KUFICHUA WATOTO WENYE ULEMAVU"

Post a Comment

Loading...