Loading...
title : WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI AMTOLEA UVIVU MKANDARASI ANAYEJENGA MATANKI YA KUHIFADHIA MAJI DAR
link : WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI AMTOLEA UVIVU MKANDARASI ANAYEJENGA MATANKI YA KUHIFADHIA MAJI DAR
WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI AMTOLEA UVIVU MKANDARASI ANAYEJENGA MATANKI YA KUHIFADHIA MAJI DAR
*Ni baada ya kuchelewesha kukamilisha mradi uliotakiwa kumalizika mwaka 2017
Na Karama Kenyunko, blogu ya Jamii
WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji Profesa Makame Mbarawa amemuagiza mkandarasi anayejenga matanki ya kuhifadhia maji na pampu na kusukumia maji kukamilisha mradi huo haraka hadi ifikapo mwishoni mwa Septemba mwaka huu
Amesema mkandarasi huyo Jain Irrigation system kutoka India hadi sasa amekamilisha asilimia 87. 5 ya mradi huo ulioanza Machi mwaka 2016 na ulipaswa kukamilika Novemba mwaka 2017.
Waziri Mbarawa ameyasema hayo leo wakati wa ziara yake ya siku tatu ya kukagua miradi ya maji inayosimamiwa na Mamlaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA) ambayo bado ipo kwenye utekelezaji katika maeneo mbalimbali jijini.
Amesema mradi wa uboreshaji wa mfumo wa usambazaji maji jijini ni wa muhimu na utagarimu Sh. bilioni 72.43 lakini inasikitisha mpaka sasa bado hajakamilisha.
"Mradi huu ni muhimu sana kwani watanzania wengi hasa wananaoishi hapa jijini Dar es Salaam wanachangamoto kubwa ya maji,"amesema Mbarawa.
Amesema lengo kubwa la kuanzishwa kwa mradi huo ilikuwa ni kuhakikisha changamoto za maji kwa watanzania zinakwisha lakini mkandarasi bado analeta shida.
Kutokana na mapungufu hayo ya Mkandarasi, Waziri Mbarawa amemuagiza Meneja mradi huo, Anil Vitankar kuhakikisha mradi huo unamalizika kwa haraka na pia amemuagiza mkandarasi huyo kuwepo kwenye eneo la mradi kwa saa 24, na kama akishindwa kumaliza mradi huo kwa wakati waliokubaliana ambao ni mwisho mwezi September basi hiyo ndio itakuwa mara yako ya mwisho kwa mkandarasi huyo kufanya kazi nchini.
WAZIRI wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mbarawa (wa pili kulia), akikagua sehemu ya kuhifadhi vifaa kwa ajili ya ujenzi wa mradi wa uboreshaji wa mifumo ya maji Dar es Salaam na Pwani, unaosimamiwa na Mamalaka ya Majisafi na Majitaka Dar es Salaam (DAWASA).
Waziri wa Maji na Umwagiliaji, Profesa Mbarawa, akitoka kukagua tenki la kuhifazia maji, Mabwepande, Dar es Salaam.
Profesa Mbarawa, akizungumza na waandishi wa habari pamoja na kumpa maagizo mkandarasi wa Kampuni ya Jain Irrigation System kutoka nchini India mara baada ya kufanya ukaguzi wa ujenzi wa mradi wa uboreshaji wa mifumo ya maji Dar es Salaam na Pwani.
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
KUSOMA ZAIDI BOFYA HAPA
Hivyo makala WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI AMTOLEA UVIVU MKANDARASI ANAYEJENGA MATANKI YA KUHIFADHIA MAJI DAR
yaani makala yote WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI AMTOLEA UVIVU MKANDARASI ANAYEJENGA MATANKI YA KUHIFADHIA MAJI DAR Wakati huu, pengine unaweza kutoa faida na wewe wote. Sawa, kuona katika post nyingine makala.
Wewe ni sasa kusoma makala WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI AMTOLEA UVIVU MKANDARASI ANAYEJENGA MATANKI YA KUHIFADHIA MAJI DAR mahali kiungo https://somalatest.blogspot.com/2018/07/waziri-wa-maji-na-umwagiliaji-amtolea.html
0 Response to "WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI AMTOLEA UVIVU MKANDARASI ANAYEJENGA MATANKI YA KUHIFADHIA MAJI DAR"
Post a Comment